Somo la 1

Watoto hawajifunzi tu wakiwa darasani, wanajifunza pia wakiwa wanacheza. Wanajifunza kutoka kwa wengine, kwa kuangalia kile wanachokifanya wengine. Hujifunza kwa kuzungumza, kuimba, kwa kukariri na kwa kushirikishana katika mazungumzo. Unaweza kutumia mchezo ili kufanya ujifunzaji katika darasa lako uwe wa mafanikio na kuziba uwazi kati ya kinachotokea darasani na nje ya darasa.

Katika Shughuli 1, wanafunzi wako wanakuwa kama watafiti, na wanakwenda kwenye uwanja wa michezo (au mahali pengine) ili kurekodi kile wanachofikiri kuwa wataweza kujifunza pale. Wanaporudi darasani wanazungumzia kile ambacho wamekigundua: Unaweza kusikiliza mazungumzo yao ili kuona kile ambacho unafikiri wanafunzi wako wamejifunza uwanjani hapo.

Uchunguzi kifani ya 1: Mwanafunzi wa miaka sita ajifunza na kufundishaKiswahili

Maria ambaye ana umri wa miaka sita anasoma katika shule ambayo

Kiswahili ni lugha inayotumika darasani, ingawa si lugha yake ya kuzaliwa.

Kila siku kwa muda wa wiki nzima, Maria aliweza kuonekana wakati wa mapumziko akiwaangalia watoto wengine wakiruka kamba. Hakujiunga, lakini alisimama karibu ili kuweza kuona na ‘kusikiliza’ wimbo ambao wanafunzi walikuwa wakiuimba. Siku ya kwanza ya wiki ya pili, Maria alikuwa kwenye ile sehemu yake ya kawaida hatua chache kutoka eneo la kuchezea, lakini sasa aliweza kusikika ‘akitoa sauti’ za maneno ya kwenye wimbo.

‘Ruu-ka, ruuu-kia ndani na seeema

Moja-aa mbili-iii, tatuuu,

Ruuu-kia na-a mimi.’

Alirudia maneno haya tena na tena, akijitahidi kuyasema kwa sauti kubwa, kwa wororo na kwa kutumia mkazo tofauti tofauti kwenye sehemu za neno. Alirudia wimbo huu mara kadhaa na kisha kuwasikiliza tena wanafunzi wengine. Alitabasamu, na kuimba tena ule wimbo.Mwishoni alitafuta kamba na kwenda kwa rafiki yake, Migueli. Aliimba ule wimbo, mstari kwa mstari, akimfundisha rafikiye huu wimbo. Alitafsiri yale maneno ya Kiswahili ili rafiki yake aweze kuelewa alichokuwa akijifunza. Kwa muda mfupi Migueli aliweza kuimba wimbo ule pamoja na Maria.

Shughuli ya 1: Kuchunguza ujifunzaji wa asili

Kabla ya kuanza shughuli hii, soma Nyenzo Rejea 2: Utafiti juu michezo ya jadi katika mtalaa . Nyenzo rejea hii inaeleza kazi moja ya utafiti na micezo miwili ambayo walimu waliibuni kama matokeo ya utafiti huo. Kusoma pia Nyenzo Rejea Muhimu: Kufanya utafiti darasani kutasaidia sana. Zungumza na wanafunzi wako kuhusu ujifunzaji. Je, wanajua kwamba daima hujifunzia: nyumbani, shuleni, wakati wanapocheza?

Liambie darasa lifanye uchunguzi katika ujifunzaji wa ‘asili’. Swali lao ni: Ujifunzaji gani unaotokea wakati watoto wanapocheza? Wanafunzi lazima waandike na kuchora kuhusu ujifunzaji wanaouona kwenye uwanja wa michezo na baada ya kutoka shule, wakati wanafunzi wengine wanapocheza, na wanapocheza wao wenyewe.

Wwaambie wanafunzi darasani washirikishane matokeo yao, kwenye vikundi. Kiambie kila kikundi kioneshe jinsi ya kucheza mchezo mmoja. Rekodi nyimbo au mikarara/viitikio wanavyoimba wakati wa mchezo, kwenye tepu, au kwa kuandika.

Waambie wanafunzi kwenye kila kikundi wajadili kile ambacho wanaweza kujifunza kutokana na michezo hii. Andika mawazo yao.

Umejifunza nini kutokana na shughuli hii inayohusu namna michezo inavyoweza kusaidia katika ujifunzaji?

Sehemu ya 3: Kutumia michezo ya jadi katika kujifunza