Sehemu ya 4: Utumizi wa hadithi na ushairi

Swali Lengwa muhimu: Unawezaje kutumia ushairi na hadithi kuhamasisha wanafunzi ili waandike?

Maneno muhimu: jina; sifa; mashairi; hadithi; wasifu, uandishi

Matokeo ya ujifunzaji

Mwishoni mwa sehemu hii, utakuwa umeweza:

  • umetumia mashairi au hadithi za majina au za kusifu ili kuchochea mawazo ya wanafunzi ya uandishi;
  • umetumia Nyenzo-rejea kama vile makala za kwenye magazeti ili kuchochea mawazo ya uandishi wa hadithi za maisha (wasifu);
  • umetalii ‘uandishi wa rasimu ’ na ‘uandishi wa kisanaa’ wakati wa kuandika.

Utangulizi

Afrika nzima, tuna utajiri wa fasihi simulizi na fasihi andishi kuhusu watu ambao bado ni muhimu au hapo zamani walikuwa muhimu kwa familia zao, jumuiya zao na nchi zao. Watu hawa hushangiliwa kupitia nyimbo na mashairi ya kuwasifu na hadithi zinazohusu maisha yao (wasifu). Kwa kutumia utajiri huu wa historia ya kitamaduni katika ufundishaji wako kunaweza kukusaidia ili kujua vitu vya kusoma kwa ajili ya lugha itakayotumika darasani na kuamsha mvuto wa wanafunzi katika uandishi.

Nyenzo Rejea 5: Wimbo wa kurukaruka maneno