Somo la 3

Tunapoandika kitu, ni muhimu tuweke wazi kile tunachotaka kukisema. Tunatakiwa tupange. Baadaye, tunaanza kuandika na kusoma kile tulichokwisha andika. Tunaweza kuamua kubadili mpangilio wa baadhi ya maneno, kuongeza, kupunguza baadhi ya maneno na kuongeza au kubadili baadhi ya taarifa. Mwishoni, tunakagua uandisha ambao si sahihi, alama za kiuakifishi/uandishi au sarufi. Kazi ya mwisho inaweza kuwa tofauti kabisa na ile rasimu yetu ya mwanzo. Tunakuwa tumefanya uandishi wetu uwe wa kisanaa.

Katika darasa, kazi moja ingeweza kukamilika (yaani iwe imeandikwa kisanaa) kabla ya kuanza kazi nyingine. Uchunguzi Kifani 3 na Shughuli Muhimu hukuonesha jinsi ya kuandaa masomo ambapo wanafunzi wanatakiwa wafanye uandishi wao uwe wa kisanaa.

Uchunguzi kifani ya 3: Kushirikiana na mwenzako ili kuwasaidia wanafunzi katika uandishi

Bibi Dorcas Mabula na Bibi Beatrice Mntambo wanafundisha wanafunzi wa darasa la 6 katika Wilaya ya Kinondoni somo la Kiingereza. Huwapatia wanafunzi maoni ya kina kuhusiana na uandishi wao, hivyo wakati mwingine walimu hawa hubaki shuleni baada ya saa za shule na kushirikiana katika kusahihisha.

Siku moja mchana, kabla ya kuanza kusahihisha wakiwa wanakunywa Maltina, wote wawili walielezana kuwa walikuwa wanajisikia kuchanganyikiwa kutokana na baadhi ya wanafunzi kupuuzia maoni na masahihisho katika madaftari yao. Marafiki hawa waliona kuwa hali hii ilikuwa inatisha, kwa sababu waligundua kuwa maoni waliyowapatia katika rasimu ya kwanza katika kazi zilizotangulia yaliwasaidia kuboresha matoleo yao ya mwisho ya kazi kwa ajili ya kuendeleza kozi zao za kitaalamu. Baadaye Dorcas aligundua kitu muhimu! Wanafunzi wake hawakupata nafasi ya kufanya kazi nyingi zinazohusiana na kazi hii ya uandishi. Badala yake, kulikuwa na mada mpya katika kila somo la uandishi.

Alipomwambia Beatrice jambo hili, rafiki yake alikubali kuwa jambo hili pia lilitokea katika darasa lake. Hivyo ndivyo walivyofundishwa walivyokuwa shuleni!

Waliamua kujaribu mkabala mpya. Wakaamua kutumia masomo kadhaa kuandika rasimu na kuandika kisanaa andiko hilohilo. Wakawapatia wanafunzi mawazo ya kuwaongoza katika uandishi wao na katika marudio ya andiko hilo. Mwanzoni, wanafunzi hawakupenda kurudia kuandika andiko hilohilo, lakini walipoona jinsi kazi zao zilivyokuwa bora, walianza kulipenda zoezi hili.

Shughuli muhimu: Kutoka kwenye uandishi wa rasimu wa mashairi/hadithi mpaka uandishi wa kisanaa

Kabla ya somo, soma rasimu za kwanza za wanafunzi na amua juu ya maswali ya jumla ya kuwauliza ili kuboresha kazi zao (angalia Nyenzo-rejea 5: Maswali kwa ajili ya wanafunzi ). Yaandike maswali haya ubaoni.

Warudishie wanafunzi rasimu zao, zikiwa na maoni ya jumla juu ya kile unachotaka kuhusu uandishi wa wanafunzi. Eleza kuwa sasa uandishi wao utakuwa wa kisanaa.  

Waambie wasome tena rasimu zao za kwanza na watumie maswali yaliyoko ubaoni katika kuandika na kuboresha rasimu za pili. 

Waambie wabadilishane na wenzao rasimu zao za pili na wapeane mapendekezo kwa ajili ya maboresho.

Waambie watumie mapendekezo haya kuandika toleo la mwisho. Zungukia darasa na toa msaada inapobidi. Wahimize watumie michoro katika uandishi wao.

Kama hakuna muda ili kumalizia shughuli hii katika muda wa kipindi darasani, waambie wanafunzi wamalizie shughuli hii nyumbani na watoe ripoti siku inayofuata.

Waulize jinsi mchakato huu wa kuandika rasimu ulivyowasaidia. Kulikuwa na maboresho yoyote katika uandishi wa wanafunzi kama matokeo ya mchakato wa wanafunzi wa uandishi wa rasimu na uandishi wa kisanaa? Unaweza kujenga mambo haya?

Ukiwa na wanafunzi wadogo au ambao hawajui sana lugha inayotumiwa darasani, ungeweza kufanya nao kazi ya kuandika rasimu na kuandika tena rasimu ya kazi rahisi kwa vipindi viwili – ukiwapatia muda katika somo ambao wataweza kutafakari kile ambacho walitaka hasa kukisema.

Nyenzo-rejea ya 1: Kuandaa masomo juu ya mashairi ya majina au ya kusifu