Nyenzo-rejea ya 1: Kuandaa masomo juu ya mashairi ya majina au ya kusifu

Usuli/welewa wa somo wa mwalimu

Amua kama unataka kuchagua mashairi/hadithi za majina au za kusifu ili kuzifanyia kazi na wanafunzi wako.

  1. Chagua mfano mmoja au zaidi kutoka Nyenzo-rejea 2 au 3 AU kutoka katika Nyenzo-rejea nyingine ulizonazo AU andika shairi au hadithi yako mwenyewe.
  2. Andika shairi (ma)/ hadithi hiyo au hadithi hizo kwenye karatasi kubwa au ubaoni ili unapozitumia darasani wanafunzi waweze kusoma chapa kubwa pamoja na wewe na baadaye waweze kurejelea mashairi na hadithi hizo wanapoandika mashairi au hadithi zao wenyewe. Kama huna karatasi kubwa, andika kwenye ubao wako.

Andaa maswali ya kuwauliza wanafunzi kuhusu shairi (ma)/hadithi. Kwa hakika, aina ya swali itategemea kile ulichokichagua.

Kwa mfano, kama utachagua shairi la Thabo, ungeweza kuanza na:

‘Unagundua nini kuhusu jinsi shairi hili lilivyoandikwa?’ (Jibu: Kila mstari umeanza kwa herufi moja ya jina la Thabo).

Ukichagua hadithi ya kusifu ya Hugh Lewin kuhusu mama yake Jafta, ungeweza kuuliza: ‘Ungependa kuwa na mama kama mama yake Jafta? Nipatie sababu ya jibu lako.’

Ukishamaliza maandalizi haya, uko tayari kufundisha masomo kuhusu mashairi na hadithi za majina na za kusifu. Wanafunzi wanapoanza kuandika, zungukia darasa ili kumsaidia yeyote ambaye atapata shida katika kuanza. Wengine watahitaji msaada wa mawazo, wengine shida ya msamiati.

Nyenzo-rejea 2 na 3 zote ni mashairi, nyimbo na hadithi za kusifu lakini lugha ni ngumu kwa baadhi yazo kuliko nyingine.

Nyenzo-rejea ya 2: Mashairi na hadithi za majina