Nyenzo-rejea ya 2: Mashairi na hadithi za majina

Nyenzo rejea ya mwalimu kwa ajili ya kupanga au kurekebisha ili kutumia na wanafunzi

Shairi la majina lililoandikwa na mwalimu nchini Tanzania:

Hanna – Jina langu la Sifa lililoandikwa na Hanna Simpassa

Fahari ya moyo wangu –

Nani alileta jina hili?

Nililipataje?

Hakuna hata mmoja katika familia aliyeliota – ila mimi!

Jina langu la Kikristo.

Wazazi wangu hawakulichagua – Nililiunda,

Zamani kabla sijawa Muislamu.

Hasina – jina linalomaanisha uzuri.

Hasina – jina langu maalumu.

Roho ziliniambia katika ndoto

Umebadilishwa dini kuwa Mkristo

Hanna ni jina lako.

Hanna – jina linalomaanisha ‘Neema, huruma na sala’.

Yeye ni wa thamani kama almasi,

Hujua thamani ya kujitoa,

Kamwe hakati tamaa,

Anapata marafiki kwa urahisi,

Furaha ni nguvu yake,

Kicheko chake ni dawa nzuri;

Mtu ambaye asili yake ni maarifa thabiti.

Yeye ni mtoto wa ulimwengu.

Hivyo nilibadilishwa dini

Hasina kuwa Hanna

Na ninajivunia jina langu

Shairi la jina lililoandikwa na mwalimu nchini Afrika Kusini

Mawazo kuhusu herufi za jina langu na Thabo X

T inasimama badala ya thabiti – Mimi ni mtu imara

H kwa ajili ya hafukasti – baba na mama yangu wana asili tofauti

A ni aminifu…

Bora

Ona nilivyo–ni mimi hasa!

Hadithi ya jina iliyoandikwa na mwalimu nchini Tanzania:

Hadithi ya kupewa jina niliyohadithiwa na Nyalupala Mtavangu

Zamani, katikati ya kiangazi, babu yangu, wakati huo alikuwa anaitwa Nyalukolo, alikwenda mtoni ili kukamilisha sherehe za matambiko. Pale mtoni alitokea simba mkubwa ambaye alikwenda kunywa maji. Mnyama huyu alimshambulia, na Nyalukolo alipambana naye. Aliwaua wanyama wengi wa mwituni na haraka alikimbilia nyumbani kumwambia baba yake kuhusu kitendo hiki cha ushujaa cha kushangaza.

Baba yake, Mungai, alituma ujumbe kijiji kizima na watu walikimbilia mtoni. Ilikuwa kweli – simba aliyekufa alikuwa amelala pale chini!

Tangu siku ile, Nyalukolo alipata heshima kutoka kwa kila mtu ambaye alijua alichokifanya. Wanaume na wanawake, vijana na wazee, walimheshimu. Katika sehemu nyingine walimtania kichinichini ‘Nyalupala’. Jina hilo la minong’ono lilimfikia baba yake, Mungai, ambaye aliamua kuita watu wa kabila lile pamoja kwa ajili ya sherehe ya kubadili jina. Nyalukolo aliitwa Nyalupala rasmi, kwa maana ya ‘simba’ katika lugha ya Kihehe.

Wakati nilipozaliwa, katikati ya karne ya 20, nilipewa jina la babu yangu. Ni jina ninalolihusisha na ushujaa na ushupavu wa mzimu wangu na ninajivunia jina hili.

Nyenzo-rejea ya 1: Kuandaa masomo juu ya mashairi ya majina au ya kusifu

Nyenzo-rejea 3: Mashairi na hadithi za kusifu