Nyenzo-rejea 3: Mashairi na hadithi za kusifu

Nyenzo rejea ya mwalimu kwa ajili ya kupanga au kurekebisha ili kutumia na wanafunzi

Shairi la Kiyoruba la kusifia chatu

Baadhi ya ushairi wa kusifu husifia wanyama au vitu kuliko watu. Hapa pana shairi kutoka kwa Wayoruba wa Naijeria. Maelezo kwa baadhi ya lugha iliyotumika yametolewa baada ya shairi hili.

Chatu

Mwana wa mfalme mwenye mikogo [Mstari 1]

Mkubwa miongoni mwa nyoka.

Wanasema chatu hana nyumba.

Nilisikia maneno haya zamani

Na nilicheka nikacheka na kucheka.

Kwani ni nani anamiliki ardhi chini ya nyasi za mlimao? [Mstari 6]

Nani anamiliki ardhi chini ya nyasi za tembo?

Nani anamiliki kinamasi – baba wa mito?

Nani anamiliki dimbwi lililosimama – baba wa maji?

Kwa sababu hawatembei kwa kuongozana [Mstari 10]

Watu wanasema kuwa nyoka hutembea tu pekee pekee.

Lakini hebu fikiria

Chukulia kipiribao atembee mbele ya wote

Hongo afuatie

Na chatu atambae akinguruma nyuma yao [Mstari 15]

Nani atakuwa jasiri

Kuwasubiri?

Tini

  1. Kutembea kwa mikogo ni kutembea kwa kujivuna – ukidhani kuwa wewe ni bora kuliko wote, kujidai. Katika mstari 1, shairi linamweleza chatu kama mtoto wa mfalme mwenye mikogo.
  2. Maswali yaliyopo kwenye mstari wa 6 hadi wa 9 inaonesha kuwa chatu ana nyumba nyingi – sehemu zote mbili; katika ardhi na kwenye maji. 
  3. Katika ubeti wa pili, shairi linaonesha kuwa wanyama na watu wengine wangeogopa sana kutembea karibu na nyoka – ndio maana nyoka ‘hutembea’ pwekepweke.

Hadithi ya kumsifu mama

Mama na Hugh Lewin

Ningependa wewe, alisema Jafta, ukutane na mama yangu. Hakuna yeyote kati ya watu ninaowafahamu ambaye ni kama mama yangu. Mama yangu ni kama ardhi – amejaa mambo mazuri, mwenye joto na nguvu, na wa rangi ya kahawia. Mama yangu ni kama jua linalochomoza alfajiri, likiangaza sehemu zenye giza na kutuamsha likitubembeleza taratibu.

Huchochea moto ili uwake na baada ya muda kila mahali panajaa harufu ya chakula, ambayo hulifanya tumbo langu lingurume na kunifanya nitake kuamka.

Jinsi jua linavyoaanza siku yake na maua yakichanua na kurusha maua hayo angani ninamkumbuka mama yangu. Kama lilivyo anga, daima yeye yuko pale. Daima unaweza kumwangalia na kumwona.

Mchana jua linapokuwa kali, hutupatia kivuli na kutuburudisha, kama mti ulioko kwenye mto. Au wakati hali ya hewa inapokuwa na joto sana na vurugu, anatupoza kama mvua ifanyavyo inapoondoa vumbi kwa njia ya mawimbi, na kunyeshea nyasi na kuzifanya tena za kijani.

Halalamiki mara kwa mara, hata katika saa mbaya. Lakini kuwa makini! Akikukamata unafanya mchezo wa kudang’anya, au kuwachokoza wadogo zako wa kike, anaweza kutoa sauti kama ya radi ya mchana na macho yake yakatoa mwanga kwenye mawingu meusi.

Mama yangu hakasiriki mara kwa mara, alisema Jafta, ila ni vema zaidi anapoimba. Anatuimbia anapopika mlo wa jioni. Kama umeshawahi kusikia hopoe akiita kwenye mahindi, basi utakuwa umeshasikia mama yangu akiimba.

Baada ya mlo wa jioni, unafuata muda wa hadithi. Kwa kiasi fulani, alisema Jafta, takriban ninampenda mama wakati huo kuliko wakati wowote – baada ya kula chakula, na pilikapilika za hapo, pindi jua linapokuchwa na kila kitu ni kitulivu na kimepoa. Hapo mama hutukumbatia na kuondoa masikitiko yetu. Tunazungumzia ya leo, ya kesho, na hasa ya kesho.

Kisha blanketi la usiku linapofunika dunia, na mwezi ukiwa juu yake, mama yangu hutufunika kwa uangalifu na kutubusu na kututakia usiku mwema; hutulaza.

Vyanzo vya asili:

Chatu imechukuliwa kutoka English Matters, Grade 7 Anthology, iliyokusanywa na Lloyd, G. & Montgomery, K.

Mama na Hugh Lewin imechukuliwa kutoka New Successful English, Reading Book, Grade 6

Nyenzo-rejea ya 2: Mashairi na hadithi za majina

Nyenzo-rejea 4: Kuandaa masomo juu ya hadithi za maisha