Nyenzo-rejea 4: Kuandaa masomo juu ya hadithi za maisha

Usuli/welewa wa somo wa mwalimu

  1. Kusanya Nyenzo-rejea utakazozihitaji. Kazi hii inaweza kuchukua muda, lakini magazeti na vichekesho unavyokusanya vinaweza kutumika kwa masomo ya lugha nyingi mbalimbali pamoja na zile za usomaji na uandishi wa hadithi za maisha. Baadhi ya wanafunzi wanaweza kuleta magazeti kutoka nyumbani, hivyo waambie waziombe familia zao ruhusa ya kuchukua magazeti hayo. Waombe wenzako na rafiki zako wakukusanyie magazeti ambayo wameshamaliza kuyasoma. Katika baadhi ya nchi, wachapishaji wa magazeti huweza kutoa msaada wa nakala za magazeti kwa shule yako. Baadhi ya AZAKI pia zina machapisho mazuri sana. Kwa mfano, makala kuhusu maisha ya Julius Nyerere yanapatikana kutoka magazeti mbalimbali ya Kitanzania na nchini Afrika Kusini ucheshi kuhusu maisha ya Nelson Mandela unapatikana katika Mfuko wa Nelson Mandela.
  2. Kabla ya kuanza masomo haya lazima uwe na vitu vya kutosha vya kusoma kuhusu aina mbalimbali za watu maarufu kwa ajili ya kufanyiwa kazi na kila kikundi cha wanafunzi.
  3. Nakili katika karatasi kubwa au ubaoni, hadithi ya maisha ya Freddy Macha (wasifu ufuatao hapa chini) AU hadithi nyingine utakayoichagua ambayo imeandikwa kwa kutumia lugha rahisi.
  4. Tengeneza orodha ya vipengele vinavyofanana vya hadithi hizi za maisha ili kuvijadili pamoja na wanafunzi wako. Hivi hujumuisha:
    • i.kwa kawaida usimulizi wa hadithi huzingatia mfuatano wa wakati toka miaka ya awali mpaka ya baadaye ya maisha ya mtu;
    • ii.hudokeza mafanikio ya maisha ya mtu;
    • iii.hutoa maelezo ya kina ya kitu fulani kinachovutia au cha kushangaza kuhusu maisha ya mtu.

Sasa uko tayari kuanza somo!

Waongoze wanafunzi wakati wanapoandika hadithi kuhusu maisha

Wakati wanafunzi wanafanya kazi katika vikundi vyao, zungukia darasa ili kukagua kama wameelewa kazi hiyo na wanaweza kupata makala za kutumia. Ungeweza kuandika ‘orodha-kaguzi’ ubaoni ili kuwaongoza wanafunzi katika uandishi wao. Kwa mfano:

jina(ma) ya mtu huyo;

sehemu aliyozaliwa;

maelezo ya familia;

‘historia’ – siku za shule, mafanikio ya awali, mafanikio ya baadaye;

Vitu vya kuvutia/vya kuhuzunisha/vya kushangaza ambavyo vimetokea katika maisha ya mtu huyo.

Wahimize wanafunzi wafikirie kuhusu utaratibu watakaoutumia ili kuandika habari za mtu huyo na kutumia maneno yao wenyewe. Wasinakili tu kutoka kwenye makala.

Hadithi ya maisha ya Freddy Macha (wasifu)

Freddy Macha alizaliwa katika miteremko ya mlima Kilimanjaro nchini Tanzania. Yeye ni mwandishi wa nathari, ushairi, tamthiliya na nyimbo, na pia ni mpiga-ala mbalimbali, mwimbaji na mwigizaji.

Akiwa na umri wa miaka 13, Freddy alianza kuimba na kuigiza jukwaani. Katika miaka ya 1970 na 1980, alikuwa anaishi na kufanya kazi kama mwandishi wa habari jijini Dar es Salaam na alikuwa na vitabu vyake alivyochapisha vikiwemo Twenzetu Ulaya (mkusanyiko wa hadithi za Kiswahili ), wasifu wa mwana muziki maarufu Remi Ongala na mkusanyiko wa mashairi yanayoitwa Papers! Papers! Papers! Freddy alishinda tuzo ya BBC ya ushairi mwaka 1981 na mashairi hayo yalitokea katika mkusanyiko Summer Fires.

Mwaka1984, Freddy alifanya ziara iliyokuwa ya mafanikio katika nchi za Skandinavia ikiwa ni pamoja na Tamasha la Kimataifa la Thieta la Oslo pamoja na kikundi chake cka Kitanzania cha Sayari. Baadaye, kwa kipindi cha miaka mine tangu 1988, Freddy alikuwa anaongoza kikundi cha bendi cha rege kilichoitwa ‘reggae-afro-funk band Os Galas’, cha Brazili.

Freddy alikwenda Uingereza mwaka 1996 na alifanya miradi mingi ikiwa ni pamoja na warsha, drama na muziki. Kwa kutembelea sehemu nyingi, Freddy huzungumza na kuigiza kwa kutumia lugha mbalimbali. Tangu 1998 mpaka 2001, katika miji ya Stoke Newington na Brixton, Freddy amefanya tamasha maarufu katika Baa ya Lorca lililoitwa Usiku wa Muziki wa Dunia ambapo wanamuziki waliweza kukutana na kujaribu vifaa vipya. Hili lilijulikana kama 'the local WOMAD' na gazeti la ‘The Hackney Gazette’ na ndiyo sababu muhimu kwa Freddy kuwa Mwakilishi wa Umoja wa Wanamuziki wa Dunia kwa upande wa sehemu ya muziki wa Jadi na wa Kimapokeo mwaka 1999–2001.

Hivi sasa, Freddy anaweza kuendesha warsha na matamasha mbalimbali mashuleni na katika kumbi za Uingereza. Alitunga kichekesho cha kitashtiti kinachoitwa ‘News No News’, ambacho wakati mwingine anakiigiza peke yake au na bendi yake ya Kitoto. Bendi ya Kitoto imeundwa na wanamuziki sita kutoka sehemu mbalimbali za Afrika, Karibiani, nchi za Uingereza na Amerika Kusini.

Nchini Uingereza, Freddy ametoa rekodi mbili: albamu inayoitwa Constipation (2000) yenye miziki 11 na wimbo mmoja unaoitwa Kilimanjaro. Constipation ina muziki, nathari na ushairi na inatumia lugha mbalimbali, ambayo imetengenezwa kutokana na utaalamu wa Freddy. Kwa mfano, kuna aina mbalimbali za nyimbo nzuri za Kiswahili na nyimbo za Kiingereza ambazo zinatoa mafunzo mazito kuhusiana na jamii. Freddy anafanya kazi sana za kutoa albamu mpya kwa ajili ya watoto wa shule. Matarajio ni kwamba albamu hiyo itakuwa bora kama Constipation.

Nyenzo-rejea 3: Mashairi na hadithi za kusifu

Sehemu ya 5: Kubadilisha hadithi simulizi, mashairi na michezo kuwa vitabu