Somo la 1

Wanafunzi wanaozungumza lugha ya nyumbani ambayo ni tofauti na wanayotumia darasani wanahitaji kujua kama unaithamini lugha yao ya nyumbani. Hii ni muhimu kwa kuwa lugha ya nyumbani ni sehemu ya mtu alivyo. Njia mojawapo ya kueleza hili ni kuwahimiza wanafunzi wako kutoa hadithi na vitendawili, kughani mashairi, kuimba nyimbo na kueleza michezo katika lugha za nyumbani na kisha kuziandika, ama kwa lugha zao za nyumbani au lugha nyinginezo.

Katika Shughuli 1, uwasaidie wanafunzi wako kugundua tofauti kati ya matini simulizi na andishi. Utawahimiza kufikiri kuhusu yaliyo na thamani katika utamaduni simulizi, kwa nini watu huandika na lugha zipi hutumika katika mazungumzo na katika maandishi.

Uchunguzi kifani ya 1: Kusimulia hadithi katika lugha za nyumbani; kuziandika katika lugha ya mawasiliano darasani

Hivi karibuni Bwana Okitikpi, mwalimu mzungumzaji wa lugha ya Kiyoruba, amehamishiwa Kaskazini mwa Nijeria katika jamii izungumzayo lugha ya Kihausa ikiwa lugha kuu, lakini baadhi ya wanafunzi wanazungumza lugha tatu za Kinijeria. Wazazi wachache na vijana watu wazima wamekubali kuwa walimu ‘wasaidizi’. Wanafahamu Kihausa na Kiingereza kidogo na wanamsaidia Bwana Okitikpi kujifunza Kihausa ili aweze kwasiliana na wanafunzi vyema. Kwa kuwa baadhi ya wanafunzi wake wanaweza kuzungumza lugha tatu za Kinijeria, Bwana Okitikpi amewahusisha wasaidizi hawa katika shughuli za utambaji wa hadithi ili kujenga kujiamini kwa wanafunzi katika uzungumzaji na kuwaonesha kuwa lugha zao za nyumbani zinathaminiwa.

Anataka wanafunzi kuandika hadithi, hususan katika lugha zao za nyumbani. Hata hivyo baadhi ya lugha hizo hazina mfumo wa maandishi, kwa hiyo ameamua waandike hadithi zao kwa kutumia lugha ya Kihausa.

Mmoja wa wasaidizi wake amejadiliana na wanafunzi kuhusu sababu za watu kuandika hadithi. Kisha, wanaandika hadithi wanayoipenda sana, kwa kutumia lugha ya Kihausa, ili waiweke katika kitabu kwa ajili ya maktaba ya darasa.

Bwana Okitikpi aliwaweka wanafunzi wake katika vikundi kwa ajili ya shughuli hii, akihakikisha kuwa angalau mwana-kikundi mmoja ni mzungumzaji mzuri wa lugha ya Kihausa na anaweza kuwasaidia wengine. Pia alimtaka msaidizi wake amsaidie kuangalia mchakato wa uandishi.

Shughuli ya 1: Uandishi wa fasihi simulizi na michezo

Kwanza, soma Nyenzo-rejea 1: Jinsi hadithi zinavyoandikwa katika vitabu, na fikiria juu ya majibu ya maswali matano kwa ajili ya wanafunzi.

Watake wanafunzi wakueleze vichwa vya habari vya hadithi, mashairi, nyimbo na michezo katika lugha za nyumbani. Viandike ubaoni.

Jadili maswali haya na wanafunzi:

Je, matini hizi za lugha ya nyumbani zimeandikwa katika vitabu? Kwa nini watu huandika hadithi, mashairi, nyimbo na michezo katika vitabu?

Ungependa hadithi, mashairi, nyimbo na michezo ya lugha yako ya nyumbani kuandikwa katika vitabu? Kwa nini iandikwe au kwa nini isiandikwe?

Ni katika lugha ipi au zipi ambazo ungeandika mashairi, hadithi na michezo katika kitabu?

Vitabu vinaandikwaje na vinatolewaje? Waambie wanafunzi watakuwa wanaandika vitabu kwa ajili ya maktaba yao ya darasa.

Watake wanafunzi kila mmoja kuchagua hadithi aipendayo na kuandika mswada wa jaribio la kwanza katika lugha aipendayo.

Umefurahia majadiliano?

Wanafunzi wamefanyaje katika shughuli hii?

Sehemu ya 5: Kubadilisha hadithi simulizi, mashairi na michezo kuwa vitabu