Somo la 2

Baadhi ya ujifunzaji, kama kujifunza kucheza ala za muziki, kutumia kompyuta au kuendesha gari, huhitaji mazoezi mengi. Kama mwalimu, unahitaji kuwapa wanafunzi nafasi ya kurudia na kufanya mazoezi ya kile walichokwishafanya kabla ili waweze kufanya maendeleo katika juhudi zao za mwanzo. Wakati ambapo Shughuli 2 katika sehemu hii inafanana na Shughuli muhimu katika Sehemu 4, marudio haya ni muhimu. Wanafunzi watajifunza kuwa uandishi ni mchakato, na kuwa hadithi, mashairi na maelekezo yao ya michezo yaliyoandikwa yatawapa wengine furaha zaidi kama zitaandikwa kwa makini.

Kuandika, kuchora vielelezo na kusoma vitabu hivi yanaweza kuchukua masomo mengi, lakini kwa kuwa shughuli hizi huwezesha nafasi nyingi za kazi za lugha , muda utatumika vizuri. Unaweza kutumia Nyenzo-rejea 2: Orodha ya kupimia ya wanafunzi ili kuwasaidia kutathmini kazi zao. Uchunguzi-kifani unaelekeza jinsi walimu wanavyoweza kuandika vitabu pamoja na wanafunzi ambao hawajapata ujuzi wa kutosha wa uandishi.

Uchunguzi kifani ya 2: Kuwasaidia wasomaji na waandishi chipukizi jinsi ya kuandika kitabu cha hadithi

Mwalimu Goodluck Nkini anawafundisha kwa pamoja wanafunzi 60 wa darasa la 1 na la 2, katika shule mojawapo karibu na mji wa Kigoma. Mwalimu mwenzake anafundisha wanafunzi 48 wa darasa la 3 na la 4. Mara kwa mara walimu hawa wawili huwakaribisha wazazi shuleni kusimulia hadithi kwa lugha ya Kiha.

Mwalimu Goodluck Nkini aliwataka wanafunzi kumsaidia kugeuza hadithi wanayoipenda, ambayo wamesaidia kuitunga, ili iwe kitabu.

Kwanza alitengeneza daftari kubwa lisiloandikwa chochote (Angalia Nyenzo-rejea 3: Kubadilisha hadithi za wanafunzi kuwa ‘kitabu kikubwa’ ).

Aliandika hadithi kwa kutumia vifungu na sentensi fupifupi. Halafu aliamua mahali ambapo kila kifungu au sentensi iwekwe wapi katika lile daftari kubwa. Alitumia rangi nyeusi pamoja na nta kuandika hadithi kwa herufi kubwa nzuri, akiacha nafasi kwa ajili ya picha.

Aliwaonesha wanafunzi kitabu darasani, na kusoma nao hadithi. Alijadiliana nao aina ya picha zilizotakiwa katika kila ukurasa. Aliwapa kila wanafunzi katika jozi vipande vya karatasi, na jozi mbili za wanafunzi walichora picha katika kila karatasi kati ya karatasi 15.

Aliwataka wanafunzi kutafuta ukurasa unaofaa kwa kila picha, na kuwasaidia kugundisha picha hizo katika kitabu.

Shughuli ya 2: Ustadi wa kuandika rasimu ya kwanza na kusanifu vitabu

Watake wanafunzi katika vikundi vya watu wanewane kusoma rasimu ya kwanza ya hadithi zao (kutoka Shughuli 1). Watake wachague rasimu mbili (kutoka katika zile nne) za kufanyia kazi katika jozi ili kuziboresha. Wanatakiwa kutumia orodha ya kupimia ya wanafunzi katika Nyenzo-rejea 2 ili kuwaelekeza jinsi ya kufanya kazi zao.

Hatua nyingine ni kuwataka waioneshe katika kundi la jozi nyingine ya wanafunzi kwa ajili ya kuiboresha. 

Sasa kusanya kazi zao na sahihisha makosa ya tahijia, sarufi na vituo vya uandishi.

Halafu vipe vikundi kitabu chao kisichoandikwa kitu chochote (Angalia Nyenzo-rejea 3) na watake wafanye yafuatayo:

  • wapange ni sentensi zipi ziwe katika kila ukurasa na michoro iwe wapi;

  • waamue jinsi ya kugawa kazi za maandishi na michoro, ili kila mwana-kundi anashiriki.

Watake waoneshe mpango wao; jadiliana nao na watake watekeleze mpango wao.

Kwa wanafunzi wadogo, mnaweza kuandika hadithi pamoja katika kitabu kikubwa na baadaye wanafunzi wanaweza kuchora kwa kila ukurasa.