Nyenzo-rejea 3: Kubadilisha hadithi za wanafunzi kuwa ‘kitabu kikubwa’

Nyenzo ya Mwalimu kwa ajili ya kupanga/kurekebisha na kutumia na wanafunzi

Utakavyohitaji

Makaratasi makubwa ya ‘kuchapia habari’ (karibu 60 sm x 85 sm)

Penseli kubwa ya nta

Penseli

Peni kubwa zenye ncha kali

Sindano kubwa ya kushonea

Kamba nyembamba

Gundi

Vipande vidogo vya karatasi zisizo na maandishi

Karatasi kubwa ya bango au chati

Mwanzo wa hadithi uliowaambia wanafunzi wako

Sehemu iliyobaki ya hadithi, ambayo wanafunzi wamekusomea

Jinsi ya kutengeneza kitabu kikubwa

Kuandika vitabu kunaweza kuwahamasisha watoto kutaka kusoma na kujiandikia zaidi. Kwa watoto wadogo, unahitaji kufanya matayarisho kabla, ukifupisha kazi wanazohusika nazo kwa kuzingatia vipengele maalum (angalia hapa chini). Kwa watoto wakubwa na kwa kuzingatia ujuzi wao, wanaweza kujifanyia kazi zaidi (kama katika Shughuli 2).

  1. Kwanza soma hadithi yote kwa makini na hakikisha ni kamili na vituo vya uandishi vimewekwa kikamilifu.
  2. Amua ni urefu wa matini kiasi gani unaotaka kuandika katika kila ukurasa wenye sehemu mbili. Kama una madarasa ya darasa la kwanza na ni mwanzo wa mwaka wa masomo, utapenda kuhakikisha kuwa hakuna zaidi ya sentensi mbili au tatu kwa kila ukurasa wenye sehemu mbili. Katika baadhi ya sehemu za hadithi huenda ukapenda kuandika aya moja. Kama unafanya kazi na wanafunzi wakubwa, unaweza kuandika zaidi.
  3. Fikiria michoro au vielelezo ambavyo unataka viambatane na matini. Hii itakusaidia kuamua ukubwa wa kitabu, na kitakuwa na kurasa ngapi. 
  4. Chukua kadi yako nyembamba, na ikunje katikati. Hili litakuwa gamba la kitabu chako. Kama kitabu kilichotengenezwa na karatasi za uchapishaji kina gamba gumu, kinadumu kwa muda mrefu.
  5. Andika hadithi yote katika karatasi zenye mistari za ukubwa wa A4 na weka matini kwa kila kurasa yenye sehemu mbili katika mstari mpya.
  6. Kunja kila karatasi mara mbili. Ziweke karatasi pamoja na hakikisha kuwa ni safi, na zinabana vizuri. Usizifungamanishe karatasi pamoja kwanza. 
  7. Sasa amua utakapotaka kuweka matini. Utaiweka kushoto kwa kila ukurasa wenye sehemu mbili zilizotandazwa? Au utaiandika kulia mwa ukurasa? Utaiandika juu ya ukurasa? Au utaiandika chini ya ukurasa? Kila ukurasa wa sehemu mbili utaonekana tofauti? Labda utaamua kuandika toka upande mmoja hadi mwingine katika ukurasa wenye sehemu mbili? Unapaswa kuamua kuhusu hili.
  8. Sasa chukua karatasi zilizokunjwa. Fanyia kazi katika meza kubwa. Tumia kalamu ya nta ya rangi nene na andika kwa unadhifu kipande cha hadithi sehemu ya nje ya karatasi ya kwanza. Andika sehemu ndogo kwa jinsi itakavyoonekana katika ukurasa wa kwanza katika kitabu ambacho ungenunua dukani. Unahitaji kitabu chako kuonekana kimeandikwa na bingwa.
  9. Chini, kwa herufi ndogo andika majina ya wanafunzi wote ambao walishiriki kuandika hadithi, au darasa lako. (Kama ni darasa zima, itakuwa vigumu kuandika majina ya wanafunzi 50 au zaidi, kwa hiyo taja darasa kama majina yote hayawezi kuenea!)
  10. Halafu, fungua ukurasa wa kwanza wa karatasi za magazeti. Huu utakuwa ukurasa wako wa kwanza ulioandikwa sehemu zote mbili. Andika sentensi au aya ya kwanza katika ukurasa huu ulioandikwa sehemu zote mbili, ukitumia kalamu ya rangi nene yenye nta. Unapaswa kuacha nafasi ya kutosha kwa ajili ya vielelezo au michoro.
  11. Unapokuwa umekwisha andika matini katika ukurasa ulioandikwa sehemu mbili, geuza ukurasa mwingine ulioandikwa sehemu mbili, na andika sentensi au virai kwa kalamu y nta ya rangi nyeusi. Endelea hivyo hadi kumalizia kuandika hadithi yote.
  12. Chukua ‘gamba’ la kitabu chako. Unahitaji kuamua ni mahali gani pa kuandika kichwa cha habari. Ni wazo zuri kuacha nafasi kwa ajili ya vielelezo. Utaandika kichwa cha habari juu, au chini? Ukifurahia jinsi kazi ilivyo, rudishia tena maandishi yaliyoandikwa kwa penseli.
  13. Ingiza vizuri karatasi za magazeti ndani ya ‘gamba’.
  14. Sasa shona karatasi pamoja na gamba la kitabu pamoja. Kuna njia tofauti ambazo unaweza kutumia kufanya jambo hili, lakini njia zifuatazo ni bora zaidi:
  15. Fungua kitabu chako ili gamba la kitabu liwe liko chini, na katikati ya kurasa zilizoandikwa sehemu mbili ziko juu. Kwa kitabu kikubwa, ni wazo zuri kuweka alama katika nafasi mbili kwenye mkunjo katikati, ambapo unaweza kushona
  16. Weka alama juu katika nusu ya mkunjo, na weka alama ya pili katika nusu ya chini. Katika kila sehemu, tengeneza alama tatu. Alama hizi ziwe na nafasi ya sentimita 4.
  17. Tunga uzi mwembamba katika sindano wenye urefu wa sentimita 50. Ingiza ncha ya sindano katikati ya seti ya alama zile tatu, katika kurasa zote pamoja na gamba lake. Vuta uzi , lakini acha kipande cha uzi chenye urefu wa kama sentimita 7 kikining’inia na fuata chati. Kata uzi ulioshikizwa katika sindano, karibu sentimita 7 kutoka mahali ulipopenyeza kwenye karatasi. Sasa funga kwa uthabiti nyuzi za sehemu zote mbili za urefu wa sentimita 7.
  18. Rudia mchakato huu nyuma ya mkunjo.
  19. Tengeneza orodha ya vielelezo unavyotaka. Amua kama unawataka wanafunzi fulani kutengeneza vielelezo, au unataka darasa lako zima kuhusishwa. Wanafunzi wanaweza kufanya vizuri wakiwa wawiliwawili kutengeneza picha. Panga jinsi ya kutengeneza michoro.
  20. Uchaguzi wa picha. Soma , pamoja na wanafunzi wako matini yote. Fungua kurasa na soma hadithi kwa sauti. Isome hadithi kwa namna ambayo itafurahisha.
  21. Waeleze wanafunzi wako kuwa unawataka kuchora picha. Usomapo hadithi kwa mara ya pili, sita kwa muda kwa kila kurasa zenye sehemu mbili na jadili kuhusu picha inayotakiwa. Wewe na darasa lako mnapofanya uamuzi kuhusu picha inayotakiwa kwa kila ukurasa, gawia kila kielelezo kwa mwanafunzi fulani, au wanafunzi wawiliwawili.

Wape muda kutengeneza picha vizuri. Wahusishe wanafunzi kushughulikia yaliyomo kwenye kitabu. Hata wanaoanza kusoma wanaweza kukariri hadithi, na wana taarifa ya kila picha inapopaswa kuwekwa. Chini ya picha hiyo, andika majina ya wanafunzi walioichora. Endelea kwa njia hii hadi picha zote zigandishwe na kuwekewa jina.

Wakati ambapo vielelezo vyote vimekwishagundishwa, soma kitabu pamoja na wanafunzi wako. Tuna hakika kuwa wewe na wanafunzi wako mtajivunia juhudi zenu.

Imerekebishwa kutoka: Umthamo 2, University of Fort Hare Distance Education Project

Nyenzo-rejea 2: Orodha ya kuhakiki kwa ajili ya wanafunzi - ili kutumika wakati wanapohariri kazi zao kwa ajili ya kitabu

Nyenzo-rejea 4: Sifa za usanifishaji wa gamba la kitabu