Somo la 1

Sisi sote tuna mitandao tofauti ya kifamilia lakini kuna sifa na miundo ambayo tunaweza kuilinganisha. Wakati wa majadiliano ya mahusiano ya kifamilia, utagundua kuwa baadhi ya wanafunzi darasani kwako wanaweza kuwa wanatoka katika miundo ya familia ilyo tofauti ukilinganisha na wengine. Utahitaji stadi maalum kuwasaidia vijana hawa ili waweze kumudu tofauti zao na kuhakikisha kuwa vijana wengine darasani nao wanakubali tofauti hizi bila kinyongo.

Madarasa makubwa huibua matatizo maalum kwa walimu-hasa wakiwa wa madarasa tofauti. Mawazo yanatolewa katika Uchunguzi kifani 1 na Shughuli 1 kuhusu jinsi ya kutalii mitandao ya kifamilia; yatumie ukiwa na madarasa yenye idadi tofauti ya wanafunzi na wakiwa katika madarasa tofauti.Mbinu zilizotumika hapa ni uwasilishaji, majadiliano ya vikundi vidogo, na kutoa mrejesho.Nyenzo-rejea muhimu: Kufanya kazi na madarasa makubwa/madarasa tofauti huibua mawazo zaidi.

Uchunguzi kifani ya 1: Kuzungumzia aina za familia na darasa kubwa

Mama Ndonga kutoka Namibia ana darasa la wanafunzi 72. Darasa linashughulikia muingiliano wa jamii na anahitaji kutumia mbinu mbalimbali kuwasaidia wanafunzi wake kutambua aina mabalimbali za familia. Anafahamu kuwa ni muhimu kuwasaidia wanafunzi wake kugundua vitu wenyewe, badala ya kuwaeleza. Anaeleza kuhusu aina mbalimbali za familia na kuwauliza wanafunzi wake maswali mbalimbali kuhusu aina hizo. Hali hiyo inamwezesha kufahamu wanafunzi wake wanajua nini na kuwafanya wazipende habari hizo. Anagundua kuwa wanafunzi watatu wa kike waliokaa nyuma ya darasa hawakujibu maswali yake, na akaamua kuzungumza nao baada ya darasa. Kwa pamoja, wanafunzi walitambua makundi mbalimbali ya kifamilia ikiwa ni pamoja na

kiini cha familia na familia za mtandao mkubwa zaidi, mzazi mmoja na familia zinazoongozwa na watoto.

Wanafunzi wamekaa katika madawati ya watu watano watano na Mwalimu Ngunda aliwaacha wakae hivyohivyo. Vikundi vya wanafunzi waliokaa kwenye madawati ya aina hiyo havifai kwa majadiliano ya vikundi, lakini pia ndio njia pekee inayotumika, hasa darasa likiwa kubwa. Vikundi hivi huwa vimechanganyika - vina wanafunzi wenye umri tofauti na uwezo tofauti.

Kila kikundi kwenye dawati kinazungumzia hali halisi ya kwao na kinatambua aina tofauti za makundi wanamoishi. Vikundi vinatoa taarifa zao na Mwalimu Ndonga anaorodhesha ubaoni aina mbalimbali za familia. Wanafunzi wananakili orodha katika madaftari yao. Wanagundua kwa kuamsha mikono idadi ya aina mbalimbali za familia katika darasa lao. Wanajadiliana katika darasa kuhusu kwa nini ni muhimu kuheshimu tofauti za kila aina ya familia.

Katika somo linalofuata, Mwalimu Ndonga anakiuliza kikundi katika dawati lilelile kwa nini tunaishi katika makundi ya kifamilia. Sababu wanazotambua zimeoneshwa katika Nyenzo-rejea 1: Sababu za kuishi katika familia. Vikundi hivi pia vinajadili kuhusu nyumba wanamoishi na jinsi zilivyotengenezwa. Mwisho, wanaandika insha fupi kuhusu familia na nyumba zao na kueleza jinsi zinavyotofautiana na mwanafunzi mwingine darasani, hasa rafiki yake.

Shughuli ya 1: Majadailiano na mrejesho kuhusu mtandao wa kifamilia

Kuhusu tendo hili, unahitaji kutayarisha somo kutalii mtandao wa kifamilia., Ili uweze kutekeleza hili unahitaji kufikiria yafuatayo:

Kama una wanafunzi wakubwa au darasa kubwa, itafaa kutumia mbinu za maelezo na mrejesho kama alivyofanya Mwalimu Ndonga. Kama wanafunzi ni wadogo unaweza kutumia makundi au darasa zima kufanya majadiliano, lakini unaweza kuona kuwa kutumia mchoroti wa familia unaweza kuwafanya wanafunzi waelewe zaidi mahusiano ya familia zao. (Taz. Nyenzo-rejea 2: Mahusiano ya kifamilia .)

Kama una wanafunzi wadogo unaweza pia kutumia igizo kifani, wakijifanya wao ndio wana familia. Itafurahisha kuona ni nani mwenye familia ya watu wengi zaidi au nani mwenye familia yenye wanawake wengi zaidi. Unaweza kuhusisha hali hiyo na kazi za uchunguzi katika masomo ya Hisabati.

Chukua tahadhari kama una familia zinazoongozwa na watoto, kwa kuwa wanaweza kujiona tofauti na na hivyo kuona aibu au kufadhaika. Utahitaji kuwapa moyo vijana hawa na kuwasaidia wajisikie vizuri. Hakikisha kuwa wanafunzi wengine hawaathiriki kuona tofauti zao na kujihisi vibaya.

Utaanzaje darasa ili kupata usikivu wao? Utataka wanafunzi wafanye shughuli gani ili kupata matokeo ya ujifunzaji wa somo?

Ukipendezwa na andalio lako la somo, lifundishe.

Sehemu ya 1: Kutambua mtandao (muingiliano) wa jamii