Somo la 3

Kuwakaribisha wanajamii shuleni kunaweza ku wasaidia wanafunzi na kuwahamasisha katika mafunzo yao na kufanya masomo yao yawe ya kufurahisha. Hali hiyo ikitekelezwa vyema itaifanya shughuli hiyo ikusaidie masomo ya stadi za maisha kuwa kamilifu kwa wanafunzi wako. Hii ni njia nzuri ya kuwatambulisha wanafunzi wako kwa baadhi ya maingiliano mbalimbali katika jamii.

Hata hivyo kuwakaribisha wanajamii kunaweza kuchukua muda kupanga-unahitaji kutambua watu wanaohusika, kufanya mipango nao na kuhakikisha kuwa wameelewa unachotaka kufanya. Inawezekana ukahitaji kutumia nyenzo-rejea kwa ajili ya wanafunzi wako ili wajifunze katika hali halisi.

Kumbuka kutathmini wanafunzi walichojifunza baada ya tukio hili. Si tu kuhusu mada ya mwalikwa, bali pia wamejifunza nini kuhusu kupanga tukio hilo. Unaweza kufanya jambo hili kwa njia mbalimbali-kuna mawazo katika Shughuli muhimu. Tazama Nyenzo-rejea muhimu: Kuwatumia wanajamii/mazingira kama Nyenzo-rejea ili kukusaidia kupanga ugeni huo.

Uchunguzi kifani ya 3: Muingiliano (mtandao) wa jamii

Mwalimu Tomasi alizungumzia muingiliano wa jamii na darasa lake la sita. Wakiwa wawili wawili, wanafunzi walizungumzia wako katika makundi yapi tofauti ya kijamii au yapi waliyajua. Waliorodhesha ubaoni makundi tofauti yote:

Ukoo/kabila

Makundi ya kidini

Maskauti wavulana/wasichana (girl guides)

Klabu ya michezo Kundi la dansi Kwaya

Kundi la huduma ya kwanza.

Baada ya kujadili kila kundi lilikuwa na wanafunzi wangapi, darasa lilipiga kura ya kumkaribisha kiongozi wa Waislamu aje kuzungumza nao. Walifanya hivyo kwa sababu kulikuwa na mwanafunzi wa Kiislamu mmoja tu na wengine walitaka kuwa na habari zaidi kuhusu Waislamu.

Kwanza mwalimu Tomasi alikwenda kwenye maktaba ya shule na kupata kitabu kinachohusu dini mbalimbali. Alijifunza kuhusu imani ya Kiislamu na kutayarisha somo kuhusu misingi ya dini ya Kiislamu. Alifanya hivyo ili darasa lipate maarifa ambayo ni msingi wa kujua waliyofundishwa na mgeni.

Wanafunzi waliandika insha fupi kuhusu imani ya Uislamu na mwalimu Tomasi aliziweka insha hizo katika meza maalum darasani ili kila mmoja azisome. Aliwaomba pia wanafunzi wake kutayarisha maswali ya kumuuliza mgeni na walikubaliana maswali mazuri ni yapi na nani wa kumuuliza mgeni.

Mgeni alipofika, alifurahi kuona kazi ya wanafunzi na kuona yapi ambayo walikuwa wakiyajua kuhusu imani ya Kiislamu. Aliwaletea sanaa za namna mbalimbali ili wazione na wanafunzi walivutiwa sana na majibu ya maswali yake na waliuliza maswali mengi zaidi.

Mwalimu Tomasi alifurahishwa na jinsi ugeni huo ulivyowahamasisha wanafunzi wake na aliamua kujaribu mbinu hiyohiyo katika masomo yao ya siku za usoni.

Shughuli muhimu: Kuwatumia wageni kuwahamasisha wanafunzi kujifunza

Bainisha wanafunzi wako wako katika makundi yapi ya kijumuiya. Unaweza kutumia mbinu aliyoitumia Mwalimu Tomasi, kwa majadiliano na darasa zima au kwa kutumia wanafunzi wachache, kwa kuzingatia idadi na umri wa wanafunzi.

  • Amua, kwa kushirikisha darasa zima, kundi lipi la kijumuiya ambalo ungependa kulijua zaidi.

  • Jitayarishe –utatakiwa kusoma zaidi.

  • Waeleze wanafunzi wako kuhusu somo husika

  • Jadili shughuli ambazo zinatakiwa kufanyika (kwa kutumia Nyenzo-rejea muhimu: Kutumia wanajamii/mazingira kama Nyenzo-rejea).

  • Wasaidie wanafunzi wako kutayarisha maswali ya kumuuliza mgeni.

  • Waulize wanafunzi wanaojitolea (au wawili wawili au kundi) wa kutimiza shughuli hizo tofauti.

  • Waongoze wanafunzi wako wanapokuwa katika mchakato wa kukamilisha shughuli hii.

  • Baada ya mgeni kuondoka, wakumbushe wanafunzi wako kuandika barua za shukrani.

  • Fanya somo la mahitimisho ambapo utatambua wanafunzi wamejifunza nini. Hili laweza kufanywa kwa namna tofauti:

  • Kwa wanafunzi wakubwa –majadiliano, kuandika hadithi, maigizo kifani, jaribio;

Kwa wanafunzi wadogo-kuchora picha, igizo kifani.

Nyenzo-rejea ya 1: Sababu za kuishi katika familia - Orodha ya darasa ya mwalimu Ndonga