Sehemu ya 2: Kuchunguza nafasi yetu katika jumuiya

Swali Lengwa muhimu: Unawezaje kutumia usimulizi wa hadithi, maarifa ya mahali husikana utamaduni husika ili kuboresha ujifunzaji?

Maneno muhimu: tamaduni; jumuiya; maigizo-kifani kifani; uvumbuzi; tabia;usimulizi wa hadithi.

Matokeo ya ujifunzaji

Mwishoni mwa sehemu hii , utakuwa umeweza:

  • kujua zaidi kuhusu jumuiya husika kwa njia ya kujifunza kwa uvumbuzi;
  • kutumia maigizo-kifani kifani katika kubainisha tabia zinazokubalika katika mazingira mbalimbali;
  • kutumia usimulizi wa hadithi ili kukuza ufahamu wa wanafunzi wa tamaduni mbalimbali.

Utangulizi

Kujifunza kwa uvumbuzi, hadithi, na maigizo-kifani kifani ni njia za kiutendaji za kutalii jumuiya mbalimbali wanamoishi wanafunzi. Njia hizi huwafanya wanafunzi wachunguze vitu wao wenyewe, jambo ambalo ni bora zaidi kuliko tu wewe kuwaambia jinsi vitu vilivyo.

Lengo la kutumia hadithi na maigizo-kifani kifani ni kuchochea mjadala na kuwasaidia wanafunzi kuangalia mienendo na tabia zao wenyewe kwa njia ambayo haitishi. Kwa kuwa matukio ya kubuni ni tofauti na mazingira halisi ya wanafunzi, wanafunzi hawa wanaweza kuona kuwa wana uhuru zaidi wa kuzungumza.

Ni muhimu kwamba masomo ya stadi za maisha yasihubiri, ila yawasaidie wanafunzi kugundua mambo wao wenyewe na kutafakari kuhusu maisha na matamanio yao. Unatakiwa uelewe kwamba wanafunzi mbalimbali

‘watavumbua’ mambo mbalimbali yanayowahusu wao wenyewe, wanafunzi wengine pamoja na maisha yao. Katika Nyenzo-rejea 1: Jumuiya ni nini? kuna tini kuhusu jumuiya.

Nyenzo-rejea 3: Igizo la kutambua mtandao wa shule