Nyenzo-rejea ya 5: Jumuiya zinazoingiliana kitamaduni

Usuli/welewa wa somo kwa mwalimu

Unavyowasaidia wanafunzi kueleza maana ya jumuiya zao, iwe ni familia zao, kijiji au shule, ni muhimu pia wajifunze kuheshimu maoni na imani mbalimbali za watu.

Wakumbushe wanafunzi kuwa wote ni watu kutoka kaya na familia mbalimbali kwa mfano wanaweza wasiweze wote kuzungumza lugha ya nyumbani au lugha mama inayofanana. Wazazi wao wanaweza kuwa na kazi tofauti tofauti; baadhi wanaweza kuwa vibarua; wengine wakulima; wachache wanaweza kuwa wafanya biashara, wauguzi n.k.

Lakini sisitiza ukweli kwamba wote ni wa jumuiya moja, yenye maslahi yale yale. Kutokana na hili, lazima waheshimu maoni ya watu wengine katika jumuiya hiyo.

Hatua ya kwanza ya kuheshimu watu wengine ni kusikiliza maoni yao na kung’amua thamani ya maoni hayo. Wanafunzi wanapojifunza kuhusu historia na imani za watu mbalimbali, wataweza kuheshimiana zaidi. Hawataogopa tofauti za kitamaduni. Pia watakuwa na welewa mkubwa wa wao ni nani.

Tofauti za kitamaduni wakati mwingine zinaweza kuwa ni vyanzo vya mgogoro ndani ya jumuiya. Ni muhimu kwa wanafunzi kwelewa sababu za mgogoro, kama vile mabishano juu umiliki wa ardhi, tabia, fedha na mahusiano. Sehemu muhimu ya elimu ya stadi za maisha ni kutafuta njia za kujaribu kuepusha mgogoro shuleni na kwenye jumuiya.

Nyenzo-rejea ya 4: Igizo kuhusu mahusiano ya kijumuiya

Nyenzo-rejea ya 6: Mgogoro katika jumuiya