Somo la 3

Katika sehemu hii utatumia mawazo ya wanafunzi kuhusu taratibu bora za tabia ili kuwasaidia kuunda kanuni zao wenyewe za darasani.

Kuwasaidia wanafunzi kuunda kundi la kanuni kwa ajili ya darasa ni njia mojawapo ya kuimarisha ushirikishwaji na uwajibikaji, hususan kama wataandika kanuni hizi wao wenyewe. Uundaji wa kanuni zao wenyewe utawasaidia kuelewa mambo yanayotarajiwa na jamii.

Kuna makundi mawili ya kanuni yanayohitaji kufikiriwa. La kwanza ni kanuni za kijamii. Hizi zinajumuisha jinsi watu wanavyowasiliana na kutendeana.

La pili ni kanuni za kujifunza. Hizi zinajumuisha jinsi wanafunzi wanavyotenda wakati wa masomo nay ale wanayoweza kuyatenda ili wasaidiane katika kujifunza na kujisomea. Kwa kuwapanga wanafunzi wafanye kazi katika makundi utawapatia fursa ya kubadilishana mawazo na kukuza zaidi tabia ya kuheshimiana.

Ni muhimu kwamba kanuni hizi zitumike kwa mwalimu; na vilevile kwa wanafunzi. Unatakiwa kuonesha mfano mzuri kwa wanafunzi wako. Ukiwaheshimu wanafunzi wako darasani, na wao watajifunza kukuheshimu.

Uchunguzi kifani ya 3: Uundaji wa sheria za mwenendo

Bi. Mambo aliwaambia wanafunzi wake wa Darasa la III kutafakari kuhusu sheria za mwenendo walizozibainisha hapo awali na kwa namna gani sheria hizi zinaweza kuwasaidia kuunda kanuni zao wenyewe za darasani.

Aliwaambia wanafunzi kutafakari kuhusu majukumu yao mbalimbali. Mambo gani wanaweza kuyafanya ili kusaidiana kutimiza majukumu hayo?Kwanza walizungumza pamoja katika makundi ya wanafunzi wawili wawili, na halafu kama darasa. Mwishowe, katika makundi madogo madogo, aliwaambia waandike sentensi kwa kutumia: ‘Tunapaswa …’

Alizungukia kila kundi na kuwaambia wanafunzi wasome sentensi moja na kueleza kwa nini wameiandika hivyo. Kwa mfano: ‘Tunapaswa kuwa kimya darasani kwa sababu itatusaidia kusikiliza vizuri’.

Kama wanafunzi wakipendekeza katika ukanushi, kwa mfano ‘Usiongee darasani’, kwa pamoja wanabadilisha kuwa katika uyakinishi: ‘Tunapaswa kusikilizana kwa makini’.

Aliridhishwa sana na majibu yao, na alikusanya sentensi zao. Siku iliyofuata, alizipitia zote tena na alichagua sentensi nane. Kisha, Bi. Mambo aliziandika ubaoni na wanafunzi walizinakili daftarini mwao kwa ajili ya kumbukumbu.

Shughuli muhimu: Kuunda kanuni za darasani

Jadili na darasa lako kwa nini tunahitaji kanuni za darasani kwa ajili ya mwenendo na kwa ajili ya masomo. Jadili kwa nini wao – na si wewe –wataandika kanuni hizo.

Waache wanafunzi, katika makundi, wajadili mapendekezo yao kuhusu kanuni za kijamii na zile za kimasomo. Waambie waandike kanuni tano kila mmoja, kwa kutumia sentensi yakinishi. Kusanya mapendekezo kuhusu kanuni za kijamii toka katika kila kundi na kisha yaandike ubaoni. Waambie walieleze darasa kwa nini kanuni hizo ni muhimu.

Andaa upigaji wa kura: mwambie kila mwanafunzi achague kanuni sita mpaka nane kutoka ubaoni. Kama una kanuni nzuri, huhitaji kuwa na nyingi kupita kiasi. Soma kwa sauti kila kanuni, na hesabu idadi ya mikono iliyonyooshwa na wanafunzi kwa kila kanuni. Andika idadi ya mikono ubaoni na bainisha zile zilizochaguliwa na wengi zaidi.

Fanya hivyo hivyo kwa kanuni za kimasomo. Andaa darasa ili kutengeneza bango la kanuni zilizoandikwa. Organise the class to make a poster of the written rules. Libandike bango hilo kwenye mlango wa darasa ili kumkumbusha kanuni hizo kila aingiaye ndani ya darasa.

Fuatilia jinsi kanuni hizo zinavyofanya kazi kwa muhula mmoja, na pitia kanuni hizo, ikiwa ni lazima kufanya hivyo. Wewe na wanafunzi mtafanyaje kuzirekebisha?

Nyenzo-rejea 1: Faida za sheria za darasa