Nyenzo-rejea 1: Faida za sheria za darasa

Taarifa za Msingi / welewa wa somo wa mwalimu

Kuna faida nyingi za kuwa na sheria zilizoundwa vema katika darasa lako. Fungu la miongozo iliyo dhahiri kuhusu ipi ni tabia nzuri na ipi ni tabia isiyokubalika katika darasa, linakusaidia kusimamia darasa vizuri zaidi. Kwa kufuata miongozo hii kama kanuni, utaweza kuzirejelea endapo zitahitajika. Hata hivyo, ili kanuni hizi ziweze kuwa faafu kwa mtazamo chanya, wanafunzi pia wanahitaji kufahamu kwa nini kanuni fulani ipo.

Miongozo hii inawasaidia wanafunzi kuelewa wanachotarajiwa wafanye. Wanafahamu tabia zipi zinatakiwa wakati wa masomo na wakati wa mapumziko. Pia wanafahamu kuhusu jinsi ya kuwasiliana na sababu za kuwasiliana. Fungu la miongozo kuhusu tabia linakurahisishia kupanga wanafunzi wakati wa kufanya shughuli za darasani. Watajua ni wakati gani wasikilize, wakati gani wazungumze, wakati gani wajibu maswali, na kadhalika. Kuwa na miongozo inayohusu tabia maana yake ni kwamba wanafunzi wanafunzi watajenga tabia ya kutendeana vizuri. Hali hii italifanya darasa liwe la amani na ushirikiano. Kwa kuwapa fursa wanafunzi waandike kanuni zao wenyewe na kuwajibika katika shughuli za darasani, utakuwa unawatia moyo waone fahari ya kujifunza. Aidha, watakuwa na nafasi kubwa ya kufuata kanuni hizo, ambazo kwa hakika, wameziandika wao wenyewe.

Hayo hapo juu yatachangia kuleta mazingira chanya ya ujifunzaji katika darasa lako. Utaweza kutumia muda mrefu zaidi katika ufundishaji na muda mfupi zaidi katika kulidhibiti na kulisimamia darasa. Wanafunzi watasikiliza vizuri darasani na watakuwa makini katika shughuli zao. Vilevile, watajifunza kusaidiana na kustahimiliana wenyewe katika masomo yao, jambo ambalo linatakiwa kuleta ubora zaidi wa mafanikio. Kwa jinsi wanavyopata maendeleo katika kujifunza kwao, watajisikia vizuri kama ilivyo kwa watu wengine, na hii itakufanya ufurahie kuendelea kuwafundisha.

Nyenzo-rejea 2: Kuwatumia viranja wa darasa