Sehemu ya 4: Kuchunguza Kujithamini

Swali Lengwa muhimu: Utatumiaje hadithi na shughuli nyingine kukuza na kutathmini kujithamini kwa wanafunzi?

Maneno muhimu: kujithamini; mahusiano; kazi za vikundi; shughuli za kijumuiya; tathmini; hadithi

Matokeo ya ujifunzaji

Mwishoni mwa sehemu hii , utakuwa umeweza:

  • umetumia shughuli na njia mbalimbali za kuwaweka wanafunzi katika vikundi ili kukuza kujithamini kwao;

  • umekuza welewa wako wa mambo yanayoweza kuathiri kujithamini;

  • umepanga shughuli yenye msingi wa kijumuiya;

  • umetumia njia za kutathmini ujifunzaji.

Utangulizi

Sehemu hii inahusika na jinsi ya kutoa utangulizi kwa wanafunzi juu ya hulka ya mahusiano mbalimbali na kuwasaidia waelewe kwamba mahusiano haya yanaweza ama kusaidia au kudhoofisha kujithamini. Athari ya mahusiano haya juu ya elimu ya wanafunzi inaweza kuwa kubwa. Ukiwa mwalimu, unao wajibu wa kujitahidi kadiri uwezavyo kutoa mazingira ya kujifunzia yenye msaada.

‘Mkataba wa Afrika wa Haki na Ustawi wa Mtoto’ (uk. 2) unasema kwamba:

‘Katika matendo yote yahusuyo mtoto yafanywayo na mtu yeyote au mamlak yoyote, maslahi bora ya mtoto yatakuwa ni zingatio la msingi…’

Washirika katika Mkataba huu watahakikisha, kwa kadiri watakavyoweza, uwezo wa kuishi, ulinzi na maendeleo ya mtoto’

Sehemu hii inaanzisha mjadala tu na wala haiingii kwa undani katika mchangamano wa mahusiano ya uonevu na tabia isiyofaa. Inatalii jinsi haya yanavyoweza kuathiri kujifunza na kujithamini kwa wanafunzi na inakupatia mwangaza kidogo katika nafasi na wajibu wako na haja ya kutafuta msaada kutoka kwa wataalamu wengine unapohusika.

Mwishowe, tunajadili jinsi unavyoweza kuhamasisha wanafunzi kufanya kazi pamoja na kuwasaidia wale wenye matatizo.

Nyenzo-rejea 2: Kuwatumia viranja wa darasa