Somo la 1

Kujithamini ni ufunguo muhimu kwa mafanikio katika maisha. Ukijihisi vyema kuhusu wewe ni nani, utajiamini zaidi katika kuungana na wengine, kupata marafiki wapya na kukabili hali mpya.Ukiwa mwalimu, una nafasi muhimu sana ya kukuza kujithamini miongoni mwa wanafunzi kwa jinsi unavyoingiliana nao. Unapaswa kuwa makini kuhusiana na hisia na mihemko ya wanafunzi, na unapaswa kuwa mwangalifu kuhusiana na mambo unayowaambia na jinsi unavyoongea nao.

Ni muhimu kuwa na mtazamo unaojenga na unaotia moyo, ukiwasifu wanafunzi kwa kazi yao nzito na mafanikio yao, na kutumia maneno ya ukarimu kila inapowezekana. Jaribu kuwakutiliza wakiwa wanatenda mema, badala ya kuwatega ili uwashike wakiwa wanatenda mabaya. Hii haimaanishi kuwa huna haja ya kuwatia nidhamu, lakini jinsi unavyofanya hivi ni muhimu ikiwa unataka kudumisha uhusiano mzuri wa kikazi nao.

Kila mara inafaa kuanza mada mpya kwa kutafiti mambo ambayo wanafunzi wako tayari wanayafahamu. Waombe mawazo juu ya kujithamini –unaweza kushangazwa na majibi mbalimbali watakayoyatoa.

Uchunguzi Kifani 1 na Shughuli 1 vinaonesha jinsi unavyoweza kutumia hadithi kwa njia mbalimbali ili kutalii wazo kama kujithamini.

Uchunguzi kifani ya 1: Kushughulikia masuala ya kujithamini

Joni Nvambo, aliye Naijeria, ana uhusiano mzuri na wanafunzi wake 36 wa darasa la nne. Siku moja, aling’amua kuwa si wanafunzi wake wote walikuwa wakichangia darasani. Baadhi walikuwa sasa wana soni na wakimya, na hawakumwuliza maswali. Aling’amua pia kuwa hili lilikuwa linaathiri alama zao. Kwa hiyo akaamua kulishughulikia tatizo hili.Kesho yake asubuhi, Joni alisimulia hadithi ya watoto watatu ili kuwasaidia waanze kufikiria wazo la kujithamini. (tazama Nyenzo-rejea 1: Hadithi juu ya kujithamini ).Kisha akaligawa darasa katika vikundi vitatu, A, B na CH, akikielekeza kila kikundi kuorodhesha sifa za mtu mwenye ama:

kujithamini vya kutosha;kujithamini kiwango cha chini; aukujithamini kupita kiasi.

Kisha, Joni aliwapanga watatuwatatu, mmoja kutoka kila kikundi, ili wabadilishane mawazo kabla ya kujadili kama darasa.Waliweza kubainisha sifa mbalimbali, na kwa nini zilikuwa nzuri au mbaya kwa watu husika. Kutokana na hili, waliweza kuzungumzia jinsi ya kupata uwiano wa kujithamini kwa kutumia shughuli kama ile iliyoko kwenye Shughuli 1.

Shughuli ya 1: Kukuza kujithamini

Tohoa Nyenzo-rejea 1 ili ikusaidie katika shughuli hii.

  • Gawa darasa katika vikundi. Vikundi hivyo viite ama A au B.

  • Uvitake vikundi vya A vimsaidie kijana mwenye kiburi abadilike awe na kujithamini kwenye uwiano.

  • Uvitake vikundi vya B vimsaidie kijana mwenye kujithamini kiwango cha chini kubadilika ili aanze kujiamini.

  • Fuatilia majadiliano ya vikundi kuhakikisha kuwa wanafunzi wote wanashiriki.

  • Baada ya dakika 15, unda vikundi kwa kuchukua mtu wa kikundi A na kumuunganisha na mwingine wa kikundi B.

  • Watake wanavikundi kulinganisha mawazo na kupeana mapendekezo.

  • Baada ya dakika kumi, fanya majadiliano ya darasa zima kuhusu mawazo ya kumsaidia mtoto mwenye kiburi na kisha yule asiyejiamini.

  • Mwisho, kama darasa, orodhesha sifa kuu za kujithamini kunakofaa na jinsi kunavyowasaidia wanafunzi kufaidiana.

Je, shughuli hii imeathiri mwenendo wa wanafunzi katika mahusiano baina yao?

Sehemu ya 4: Kuchunguza Kujithamini