Nyenzo-rejea 1: Hadithi juu ya kujithamini

Nyenzo-rejea ya mwalimu kwa ajili ya kupanga au kutohoa kwa matumizi na wanafunzi

Kulikuwa watoto watatu walioishi katika kijiji kimoja – wavulana wawili na msichana mmoja. Siku moja, wote walianza kwenda shule. Kwa kuwa walikuwa na umri sawa, waliingia katika darasa lilelile, ingawa walipokea mambo kwa kutofautiana sana.

Mvulana wa kwanza alikuwa na akili, na alianza kufanya vizuri shuleni. Aliweza kujibu maswali mengi na mara zote alipata alama nzuri. Kwa sababu hii, alianza kujiona. Hakutaka kusikiliza mawazo ya watu wengine. Akawa jeuri, na akafikiri alifahamu kila kitu. Alikuwa na dharau kwa wengine, na akaanza kupoteza marafiki.

Mvulana wa pili aliiona shule kuwa ngumu, na hakuelewa baadhi ya mambo. Lakini aliogopa kumuuliza mwalimu kwa kuogopa kuadhibiwa. Akabaki nyuma kabisa katika masomo yake. Kwa sababu hii, akajiona hafai. Alidhani kuwa wenzake darasani walikuwa wakimcheka. Alijiona hana faida, na akadhani anadharauliwa na mwalimu, kwa hiyo hakuongea darasani.

Msichana alifurahia kwenda shule toka mwanzo. Alipenda kufanya urafiki na wenzake, na akang’amua kuwa angejifunza mengi kwao. Alikuwa na uwezo mzuri wa kujifunza lakini alipenda kubadilishana mawazo na wengine. Alipenda kuwasikiliza wengine. Alikuwa mcheshi, lakini alijifunza kutopiga sana kelele. Aliweza kuuliza maswali ilipohitajika, lakini hakujua kudai usikivu kwa yeyote.

Nyenzo-rejea 2: Aina za unyanyasaji