Nyenzo-rejea 2: Aina za unyanyasaji

Usuli / dokezo kwa mwalimu

Kuna aina mbalimbali za unyanyasaji – wa kimwili, kingono, kihisia na kisaikolojia. Aina hizi zinaweza kutokea baina ya watu wazima, baina ya watoto, au baina ya watu wazima na watoto.

Ni muhimu kwamba wanafunzi wako wawe na utambuzi wa aina hizi za unyanyasaji, kwa sababu wakiwa bado ni watoto kuna uwezekano mkubwa wa kudhurika. Huwaamini watu wazima, na kwa kawaida hufanya wanayowaambia, lakini wanapaswa kujua kwamba si kila kitu ambacho mtu mzima hufanya ni sahihi.

Unyanyasaji wa kimwili unahusisha kupiga mtu. Si lazima kuwe kwa nguvu, lakini kama unyanyasaji wa kimwili ni wa mara kwa mara unaweza kuwa na athari mbaya kwenye uhusiano.

Unyanyasaji wa kingono ni utumizi usiofaa wa mtu mwingine kwa nia ya kukidhi tamaa ya ngono, kwa kawaida bila kibali au kwa shinikizo la kisaikolojia au utumizi wa nguvu. Hii hutokea baina ya watu wazima, baina ya watu wazima na watoto, na pia baina ya watoto wanaoingia utu uzima. Fadhaa na madhara ya kisaikolojia yaweza kuwa mabaya kabisa, na wanafunzi wanaweza kuwa wagomvi sana au wakimya sana; wanaweza kuwa na wasiwasi wawapo na watu wazima au kuwa na mwenendo usiofaa na wanafunzi wenzao.

Unyanyasaji wa kihisia na kisaikolojia unahusisha kumtendea mtu kikatili kwa muda mrefu, hali inayomfanya ahuzunike na kusikitika. Unaweza kuhusisha kumtukana au kumkosea adabu, au kudhoofisha kujiamini kwake na kudunisha mafanikio yao.

Kuna mifano mingine pia, kwa mfano unyanyaswaji na wazazi. Huu unaweza kutokea, kwa mfano, kama baba atamrubuni mtoto wake wa kiume kwa kumwekea sigara mdomoni na kumwashia.

Unyanyaswaji wa namna hii pia waweza kuwa kumpiga mtoto kila mara na kwa nguvu na kumpatia majeraha na kumkandamiza na kumdhibiti kupita kiasi.

Kunaweza kuwa na unyanyasaji wa nyumbani – udhalilishaji wa wake au wafanyakazi wa nyumbani, hata kama wanafanya kazi kwa juhudi.

Unyanyasaji wa namna hii husababisha maumivu ya kimwili na kihisia, na yanaweza kusababisha huzuni na kutojiamini sana.

Nyenzo-rejea 1: Hadithi juu ya kujithamini

Nyenzo-rejea 3: Dhima ya walimu