Nyenzo-rejea 4: Kutafiti mambo ambayo wanafunzi wanafahamu kuhusu mahusiano

Nyenzo ya mwalimu kwa ajili ya kupanga au kutohoa kwa ajili ya matumizi na wanafunzi

Rehema ni mwalimu mchapakazi kwenye shule ya jumuiya iliyopangiliwa vizuri katika kijiji katikati ya Tanzania. Kwa mkabala wake bainifu na kamilifu wa ufundishaji, alirahisisha maneno magumu ambayo wanafunzi wake wangeweza kukutana nayo katika uchunguzi wao wa mahusiano. Nia ni kuwahamasisha na kusaidia welewa wao.

Rehema anawataka wanafunzi wake wajadiliane katika vikundi:

  • kina nani wanahusiana nao kila siku nyumbani, na kwa nini;

  • kina nani wanabadilishana mawazo na uzoevu shuleni, na kwa sababu gani; 

  • kama wanahusiana na walimu wao, na kwa nini.

Baada ya kujadili mawazo haya katika vikundi, na kama darasa, mwalimu anawauliza kitu kinachofanya wahusiane na mchuuzi aliye nje ya lango la shule. Anawataka wafikirie watu gani katika jumuiya wanaowaona mara kwa mara, na kwa nini.

Wanajadili mawazo haya katika vikundi; kisha wanayajadili kama darasa. Kutokana na haya, Rehema anaweza kuwasaidia wanafunzi kuanza kutambua aina mbalimbali za mahusiano waliyo nayo na watu, na mienendo inayofaa kwa kila mojawapo.

Alitumia pia shughuli ifuatayo ya vikundi kuwasaidia wanafunzi wake kutalii mawazo kuhusu mahusiano.

  • Ligawe darasa lako katika vikundi unavyoweza kuvisimamia vizuri kwa kuzingatia mchanganyiko wa jinsia, aina za haiba na ujuzi, ili viyafanyie kazi maswali yafuatayo.

  • Kiruhusu kila kikundi kuchagua kiongozi wa kupanga kazi, na mwandishi wa kuandika mawazo yao.

  • Bainisha kwamba kazi ni ya dakika 15 tu na kila kikundi kitatoa taarifa kwa dakika tano.

  • Zungukazunguka chumbani kufuatilia maendeleo ya kila kikundi na kuhakikisha kwamba kila mwanakikundi anashiriki kikamilifu na wenzake.

  • Baada ya dakika 15, viite vikundi kwa zamu kutoa taarifa, wakati vikundi vingine vikiandika tini.

  • Ukishirikiana na wanafunzi, fanya muhtasari wa mawazo muhimu kwa ajili ya wanafunzi kuandika. Waelekeze wazingatie aina mbalimbali za mahusiano na kwa nini zipo.

Maswali kuhusu mahusiano

  • Una hisia gani kwa kaya/familia ambamo ulizaliwa?

  • Una hisia gani kwa dada/kaka yako nyumbani katika familia?

  • Ni kitu gani ambacho dada/kaka yako hukufanyia kinachomfanya awe karibu nawe?

  • Nani rafiki yako bora shuleni?

  • Kitu gani kinamfanya awe rafiki yako bora?

  • Kitu gani kinakufanya uhusiane na mwalimu wako?

Nyenzo-rejea 3: Dhima ya walimu

Nyenzo-rejea 5: Jinsi Igizo kifani Lilivyopokewa