Nyenzo-rejea 1: Mgogoro wa kifamilia

Nyenzo-rejea ya mwalimu kwa ajili ya kupanga au kutohoa kwa matumizi na wanafunzi

Katika familia ya Kisongo, mume alikuwa akitoa fedha kwa ajili ya matumizi ya familia kila wiki. Siku moja, baba alimweleza mama kuwa hakuwa na fedha za kutosha kwa ajili ya kutoshelezea mahitaji yake. Mama hakutaka kumsikiliza baba. Alitoka chumbani kwa hasira na kubamiza mlango nyuma yake.

Asubuhi iliyofuata, hali ya nyumbani ilikuwa mbaya, kwani mama hakusikiliza maelezo ya baba. Baba aliendelea kujaribu kumweleza mama kwa nini hakuwa na fedha za kutosha, lakini mama hakumsikiliza.

Baada ya muda, baba aliwaomba watoto wazungumze na mama yao. Walifanya hivyo kwa kumwambia mama yao awe na subira. Mama aliwasikiliza na alikubali.

Mama alisikiliza kwa makini na alielewa kwa nini wiki hii baba hakuwa na fedha za kutosha – alilazimika kumkopesha kaka yake kiasi cha pesa kwa ajili ya kuwalipia watoto wake karo.

Mama aliposikia hivi, alilielewa tatizo lile. Lakini kwa upande wake, aliomba kwamba fedha kwa ajili ya chakula cha familia lazima zitengwe pembeni kabla ya kitu cho chote hakijatolewa kwa wengine, na pia ziongezwe kidogo ili kukidhi gharama za upandaji wa vyakula. Baba alikubali.

Hali ya wasiwasi nyumbani ilikwisha na kila mtu aliondoka nyumbani kwenda kwenye shughuli zake za kila siku akiwa na furaha. Mama alimkumbatia na kumbusu baba. Baba alitabasamu. Uhusiano uliokuwepo katika familia ulirudia kama kawaida

Nyenzo-rejea 2: Mgogoro wa ng’ombe wasababisha mapambano makali mwaka 2001’