Nyenzo-rejea ya 1: Kitu ambacho waandishi na wasomaji wafanisi wanatakiwa kukijua

Nyenzo-rejea ya mwalimu kwa ajili kupanga au kurekebisha ili kutumia na wanafunzi

Chagua hadithi yenye wahusika na matukio ambayo unafikiri yatawasisimua wanafunzi wako.

Fikiria maelezo ya usuli ambayo wanafunzi watayahitaji ili waelewe na wafurahie hadithi. Amua jinsi utakavyoyatoa kabla ya kuanza usomaji wa hadithi. Kwa mfano, wanafunzi wenye umri mdogo katika baadhi ya sehemu za Afrika watamfahamu kiboko, lakini wengine wanaweza wasielewe, hivyo kabla ya kusoma hadithi ya Kiboko Mkali utatakiwa uchunguze wanafunzi wanajua nini kwa njia ya kuwauliza maswali kama haya:

Maswali ya kujua maarifa waliyo nayo

  • Kiboko anafananaje?
  • Je, kiboko anaweza kukuogopesha? Kwa nini ni ‘ndiyo’ , au kwa nini ni ‘hapana’?
  • Unaweza kumwona kiboko wapi?
  • Kiboko anakula nini? Swali la kwanza linalotabirika
  • Hadithi hii inaitwa Kiboko Mkali. Angalia mchoro kwenye jalada la mbele. (Mchoro unaonesha kiboko akijaribu kujikinga kwa majani ya jamii ya mchikichi.) Unafikiri hadithi itahusu nini?
Imechukuliwa kutoka: Dixie Elementary Magnet School, Book Jackets; Website

Angalizo: Wakati maswali haya yanarejelea hadithi ya Kiboko Mkali, maswali hayahaya yanaweza kuwahusu wanyama, watu, mahali au shughuli zinazohusiana na hadithi yoyote ile.

Fanya mazoezi ya kusoma hadithi kwa sauti kabla ya kuitumia kwenye darasa lako. Fikiria jinsi ya kuigiza sauti za wahusika na vitendo utakavyoweza kuvitumia ili hadithi ionekane kama ya kweli. Kama kwenye hadithi kuna michoro, amua namna ya kuitumia utakapokuwa unasoma hadithi hii darasani kwako.

Angalia sehemu za hadithi ambazo wanafunzi wanaweza kushiriki mara tu watakapoifahamu hadithi hii. Kwa mfano, katika hadithi moja, Tembo Eddie alijaribu kuigiza vitendo vya wanyama wengine au vitendo vya binadamu na kila mara ashindwapo hulia ‘Wah! Wah! Wah! Boo! Hoo! Hoo! Natamani ningejua kitu ambacho ninaweza kufanya!’ Unaweza kuandika kiitikio kama hiki ubaoni kwako ili wanafunzi waweze kufuatilia.

Tafuta mahali kwenye hadithi ambapo unaweza kuwauliza wanafunzi baadhi ya maswali ya utabiri kama vile: ‘Unafikiri Eddie atafanya nini baadaye?’ au ‘Kiboko Mkali atatatuaje tatizo lake?’

Nyenzo-rejea ya 2: Maswali ya kutumia wakati wa usomaji wa kitabu – usomaji wa kwanza, wa pili na wa tatu