Somo la 1

Mazoezi ya ufahamu ni ya kawaida sana, lakini yanasaidiaje stadi za usomaji wa mwanafunzi?

Uchunguzi kifani 1 inaonesha kuwa unahitaji kufikiri kwa makini hasa kama kweli maswali ya ufahamu katika usomaji wa vitabu yanasaidia kujua wanachoelewa wanafunzi kutokana na usomaji huo. Unahitaji kutunga maswali au shughuli ambazo zinahitaji wanafunzi kusoma taarifa za matini kwa uangalifu. Shughuli 1 inakuonesha mifano ya kujaribu na kuitumia wakati unapotunga maswali yako na shughuli nyinginezo. Nyenzo Rejea Muhimu: Kutumia maswali ili kusaidia kufikiri inakupa mawazo zaidi.

Uchunguzi kifani ya 1: Kufiria upya kuhusu ‘ufahamu katika usomaji’

Katika warsha huko mjini Lusaka, Zambia, walimu wa Kiingereza kama lugha ya nyongeza walisoma matini ambayo haina maana na kujibu maswali kuhusu matini hiyo. Sentensi ya kwanza katika matini hii ilikuwa: ‘Some glibbericks were ogging blops onto a mung’ na swali la ufahamu lilikuwa nani alikuwa ‘ogging blops onto a mung?’ Kila mwalimu alijua jibu ‘some glibbericks’ . Katika majadiliano yao, waligundua kuwa wangeweza kutoa jibu sahihi kwa sababu walijua kuwa katika Kiingereza ‘some glibbericks’ ilikuwa ni kiima cha sentensi. Hawakuhitaji kujua nani au ‘glibberick’ kilikuwa ni kitu gani ili kutoa jawabu!

Baada ya majadiliano, walifanya kazi katika vikundi, ya kutunga maswali na kazi nyinginezo ambazo zingewaonesha kama wanafunzi wanaelewa au hawelewi matini iliyotumika katika kazi hizi. Walijifunza kuwa maswali yasiruhusu wanafunzi kunakili tu taarifa ya sentensi moja katika matini.

Walitayarisha kazi ambapo wanafunzi walijaza jedwali, walitengeneza bango au kutayarisha muhtasari wa kutumia katika mdahalo kama njia ya kuonesha walichojifunza kutoka katika matini waliosoma.

Walitafakari kuwa maswali waliyouliza na shughuli nyingine walizotayarisha zilimaanisha kuwa waliweza kutathmini welewa wa wanafunzi.

Shughuli ya 1: Kufahamu na Kupokea taarifa za matini

Soma Nyenzo rejea 1: Matini kuhusu takataka . Toa nakala za makala na kazi au andika aya na kazi ubaoni.

Zifunike.

Kabla ya wanafunzi kusoma makala, uliza maswali ya utangulizi. Maswali yako yawasaidie wanafunzi kuoanisha wanayoyajua na taarifa mpya iliyomo katika matini (Angalia Nyenzo rejea 2: Maswali ya utangulizi ). Kama wanafunzi ni wenye umri mdogo au unahitaji kuwasomea matini, unaweza kuandika majibu yao ubaoni.

Baada ya hapo, funua makala na kazi ulizotayarisha, na kuwataka wanafunzi wasome makala hiyo kimya na kuandika majibu ya kazi hizo. Watakapokuwa wamemaliza, kusanya vitabu vyao na tathmini majibu yao

Rudisha vitabu na /au toa maoni yako kwa darasa zima kuhusu waliyofanya vizuri na jadili matatizo yoyote waliyokumbana nayo. Angalia majibu ya kazi hii yaliyopendekezwa katika Nyenzo rejea 1 )

Katika somo linalofuata, watake wanafunzi wafanye kazi katika makundi madogo madogo kutengeneza bango linalokataza utupaji ovyo wa takataka na lioneshe darasani (Angalia Nyenzo rejea 3: Mabango mazuri ).

Sehemu ya 3: Njia za Usomaji na upokeaji wa taarifa za matini