Somo la 3

Kujifunza kutafuta na kufanya muhtasari wa mawazo makuu kutoka katika sura za vitabu na vitini vingine kunakuwa muhimu kwa wanafunzi kwa jinsi wanavyopanda madarasa shuleni. Stadi hizi zinahitaji mazoezi kuzimudu.

Shughuli Muhimu na Nyenzo rejea 5: matini kuhusu mbuyu inatoa mifano ya njia ya kuwasaidia wanafunzi jinsi ya kufanya muhtasari wa taarifa za matini. Utahitaji kufanya shughuli hiyo mara nyingi. Kwa wanafunzi wakubwa, unaweza kuwaomba wenzako kukuonesha wanafunzi unaowafundisha wanahitaji kusoma nini katika masomo mengine kama vile masomo ya jamii au sayansi. Baadaye unaweza kutumia aya kutoka masomo ya fani ya jamii au vitabu vya sayansi kwa ajili ya kufanya kazi ya muhtasari katika somo la lugha kwa kufuata hatua zilizomo katika Shughuli Muhimu.

Uchunguzi kifani ya 3: Kufupisha mawazo muhimu kutoka katika sura za vitabu

Wanafunzi wa darasa la Mwalimu Emmanuel Chadwali walikuwa na wasiwasi kuhusu mitihani inayofuata. Walimwambia kuwa hawelewi walimu wao walimaanisha nini walipowaambia kupitia (kudurusu) sura za vitabu vyao. Emmanuel aliamua kutumia matini ya taarifa kutoka katika kitabu cha Kiingereza ili kuwapa wanafunzi wake baadhi ya mawazo kuhusu jinsi ya kutafuta na kuandika mawazo muhimu ya matini.

Aliwauliza wanafunzi wake kumwambia shabaha ya jedwali la yaliyomo, vichwa vya sura na sura ndogo katika vitabu vyao. Ilikuwa wazi kutokana na ukimya wao kwamba wanafunzi wengi walikuwa hawajawahi kufikiria jambo hilo. Wachache waliweza kusema kuwa majedwali haya humsaidia msomaji kupata mawazo kuhusu mada muhimu za kitabu. Emmanuel aliwaambia wanafunzi kuwa ili kusoma tena sura, wanapaswa kuandika vichwa vya habari katika ukurasa, wakiacha nafasi kati ya kichwa kimoja na kingine, wafunike daftari zao na kujaribu kuandika mawazo muhimu katika yale waliyosoma.

Baadaye, wanapaswa kucheki maelezo yao waliyoandika dhidi ya mawazo yaliyomo katika kitabu na kufanya masahihisho katika maandishi yao kwa kuongezea chochote muhimu walichosahau au wafute kile ambacho wameandika kwa makosa. Emmanuel alisema kuwa wanafunzi wengine hupendelea kuandika mawazo yao kwa njia ya michoro ya ramani ya mawazo ambapo kuna uhusiano wa mawazo muhimu. (Angalia Nyenzo rejea 5 na Nyenzo-rejea Muhimu: Kutumia ramani ya mawazo na)

Mwisho, aliwakumbusha kuwauliza walimu wao kuelezea chochote ambacho hawakukielewa. Emmanuel aliwaelezea pia jinsi alivyoandika kumbukumbu kuhusu mambo ya wanafunzi wake aliyoyagundua na ujifunzaji wao ili kumsaidia kupanga masomo zaidi.

Shughuli muhimu: Kuboresha stadi za kuandika muhtasari

Kabla ya somo , nakili matini kutoka Nyenzo rejea 5katika mbuyu au iandike ubaoni. Jaribu shughuli hizo kabla.

Kwa kuwaonesha wanafunzi kurasa za magazeti na majarida, waulize kwa nini matini yana vichwa vya habari na yanawaambia nini wasomaji wake.Watake wapendekeze kwa nini vitabu vyao vina vichwa vya habari na vichwa vidogo vya habari.

Watake wanafunzi wasome matini ya taarifa kuhusu mbuyu na kufanya kazi katika jozi kuamua ni aya zipi zinajadili mada ileile. Watake waandike kichwa cha habari kinachofupisha aya kwa kila mada. Watake baadhi ya wanafunzi wako kusoma kwa sauti vichwa vyao vya habari na kuviandika ubaoni.

Kubalianeni ni vichwa vipi bora vya habari kwa kila aya vinavyohusu mada ileile. Viache vichwa vya habari bora ubaoni ukiacha nafasi kwa kila kimoja. Watake wanafunzi washauri mawazo muhimu kutoka kwenye aya na kuyarekodi. Waonesha wanafunzi jinsi ya kuhusisha vichwa vya habari na mawazo muhimu katika ramani ya mawazo ili kuwasaidia kukumbuka kuhusu mbuyu.

Nyenzo-rejea ya 1: Matini kuhusu takataka