Nyenzo rejea 5: Matini kuhusu mbuyu

Nyenzo-rejea ya mwalimu kwa ajili kupanga au kurekebisha ili kutumia na wanafunzi

Kabla hujaanza Shughuli muhimu, unaweza kutumia Nyenzo rejea 1 kama mfano na kujadiliana na wanafunzi wako jinsi vichwa vidogo vya habari vinavyoweza kufanya muhtasari wa mawazo muhimu.

Mbuyu

Mbuyu sio mti wa kawaida. Baadhi ya watu hufikiria kuwa ni mbaya kwa kuwa ni mnene na muda mwingi huwa hauna majani. Unaonekana pia kutukua kwa utaratibu mzuri juu. Kwa hakika baadhi ya watu wanaishi katika sehemu ambazo kuna miti hii wanasema kuwa hukua kinyume matawi yake yakiwa ardhini na mizizi yake ikiwa juu.

Mbuyu unafanya vitu tofauti ukilinganisha na miti mingine. Miti mingi hushiriki mchavuko kwa kusaidiwa na nyuki na ndege ambao huchukua punje za chavua toka mti mmoja hadi mwingine ili miti irutubishwe na kutengeneza maua mengine, matunda au kokwa. Mibuyu husaidiwa na popo. Wakati wa mwanzo wa kiangazi mti huu hutoa maua makubwa yenye petali.

Maua huchanua usiku wakati popo wanapotokea. Popo hufyonza nekta na husafirisha chavua kutoka mti mmoja hadi mwingine katika mabawa yao na mwilini.

Mbuyu huishi kwa muda mrefu. Baadhi ya mibuyu mikubwa inaweza kuwa na umri wa miaka zaidi ya 3,000. 

Mbuyu una matumizi mengi. Miaka iliyopita baadhi ya watu wa kabila la Khoi na San wa Afrika ya kusini walitumia mibuyu kujengea nyumba. Waliweka moto ndani ya mti wa mbuyu ili kulainisha sehemu za ndani ya mti, na kutengeneza tundu ambamo waliishi. Pamoja na kuwa na shimo kubwa ndani, mti huo uliendelea kukua.

Ganda la mti lina matumizi mengi. Linaweza kutumiwa kutengeneza zulia, karatasi na uzi. Unyuzi wa ganda unatengeneza kamba ngumu.

Sehemu nyingine za mti zina matumizi mengine. Mizizi ikisagwa, inatengeneza uji laini. Sehemu laini ya ndani ni kinywaji cha wanyama wenye kiu wakati wa majira ya ukame . Mbegu zikivundikwa majini kwa siku kadhaa, zinakuwa dawa za kutibu homa. Majani yakikaushwa na kusagwa, yanatengeneza kahawa nzuri lakini chungu. Majani yakichemshwa yanafanana kama kabeji na yanaweza kuliwa. Nchini Tanzania, wakati mwingine maganda yakisagwa yanatumika kama dawa ya kusugulia meno.

Kuna hadithi nyingi kuhusu mbuyu. Watu wa Venda Afrika ya kusini wanasema kuwa miti hii ilikuwa ni mahali pa maficho ya mizimu. Halafu mungu alikuja na kuchimbua miti hiyo toka ardhini na kuipanda upya kinyume, yaani mizizi juu na matawi chini. Kutokana na kitendo hicho, mizimu haikuweza kujificha katika miti hiyo.

Watu wengine husema kuwa ukifyonza mbegu hutashambuliwa na mamba, na ukinywa kinywaji kilichotengenezwa kutokana na maganda ya mbuyu utakua hadi kuwa mtu mkubwa na mwenye nguvu (cheo.) Mbuyu ni mti wa maajabu. Ni mmojawapo wa miujiza ya Afrika.

Vichwa vidogo vya habari vilivyopendekezwa kwa ajili ya matini ya mbuyu

Aya 1: Mbuyu hufananaje?

Aya 2: Jinsi poleni zinavyosafirishwa kati ya miti ya mbuyu?

Aya 3: Maisha ya mbuyu

Aya 4, 5, 6: Matumizi ya mbuyu

Aya 7, 8: Hadithi na imani kuhusu mibuyu

Zingatia: Hakuna taarifa katika aya ya mwisho. Aya hiyo inaonesha angalizo la mwandishi, akitoa maoni yake kuhusu mti huo.

Muhtasari wa ramani ya mawazo ya mbuyu

Imechukuliwa kutoka: Ellis, R. & Murray, S. Let’s Use English, Learners’ Book 5

Nyenzo-rejea 4: Chati ya pai

Sehemu ya 4: Njia za kuwasilisha mtazamo wako