Nyenzo-rejea ya 3: Muundo wa hotuba za mdahalo

Usuli/taarifa ya mwanzo/uelewa wa mwalimu

Maelezo ya hoja

Bungeni, au katika kamati muhimu, wakati wajumbe wanatoa maamuzi, mmoja anaweza kutoa hoja ya kujadiliwa. Hoja ni tamko kuhusu kitu kinachopaswa kufanywa au kujadiliwa. Mdahalo unatalii sehemu zote za mjadala. Kwa mfano, kama mbunge akisimama na kusema: ‘Natoa hoja kuwa adhabu ya viboko ifutwe,’ wazo hili linajadiliwa na uamuzi unafikiwa, ambao unatoa suluhisho linalotakiwa kutekelezwa au kutotekelezwa.

Taarifa zifuatazo ni mifano ya masuala unayoweza kutumia shuleni. Unaweza kurekebisha hizi kwa kutegemea ukubwa wa darasa lako na umri wa wanafunzi wako.

Wazazi wasitumie adhabu ya viboko kuwafundisha nidhamu watoto. Tunayojifunza nyumbani ni muhimu kuliko tunayojifunza shuleni.

a) Wanaounga mkono mada ya mdahalo

Eleza mada: Nakubaliana na hoja kuwa vijana wote walio nje ya shule, wanatengwa kwa sababu ya vizingiti vya kujifunza, warudishwe shuleni.

Fafanua istilahi. Katika hali hii utahitaji kueleza una maana gani unaposema vijana walio ‘nje ya shule’, na vizingiti vya kujifunza. (Hili linapaswa kufanywa na mzungumzaji wa kwanza)

Toa sababu za kuunga mkono mada: k.m. sababu yangu ya kwanza katika kuunga mkono mada hii ni........

Sababu ya pili, …

Sababu ya tatu, …

Fanya hitimisho ya sababu zako za kuunga mkono mada: Kwa ufupi au kwa kuhitimisha ....

Eleza tena mada ya mdahalo: Kwa hiyo narudia tena au kwa hiyo nawasihi nyote kuunga mkono mada ambayo inasema kuwa.......

b) Wanaopinga mada ya mdahalo

Eleza msimamo wako kuhusu mada: Napinga mada inayosema kuwa........AU Nawaunga mkono wanaopinga mada kwamba........

Fafanua istilahi. Katika hali hii utahitaji kueleza una maana gani unaposema vijana walio ‘nje ya shule’, na vizingiti vya kujifunza. (Hili linapaswa kufanywa na mzungumzaji wa kwanza). Wote wanaohusika wanahitaji kukubali ufafanuzi wa istilahi.

Toa sababu zako za kupinga mada: k.m. sababu ya kwanza ya kupinga mada hii ni...

Sababu ya pili,...

Sababu ya tatu, …

Fanya hitimisho la sababu zako za kupinga mada: Kwa ufupi au kwa kuhitimisha...

Eleza tena msimamo wako: Ninarudia tena AU ninawasihi nyote kutounga mkono mada inayodai kuwa .........

Nyenzo-rejea ya 2: Michezo inayohimiza uelewa wa ulemavu wa viungo

Nyenzo-rejea ya 4: Sheria na taratibu za kuendesha mdahalo