Nyenzo-rejea ya 1: Uulizaji wa maswali – kuwahimiza wanafunzi kufikiri kwa umakinifu kuhusu hadithi

Nyenzo ya Mwalimu kwa ajili ya kupanga/kurekebisha na kutumia na wanafunzi

Mfano A: Hadithi kuhusu familia

Unaweza kuuliza maswali kama:

  • Ni wanafamilia wapi waliomo katika hadithi?

  • Wapi wanaonekana muhimu? Unawatambuaje?

  • Je, familia yako inafanana na hii? Kama hivyo ndivyo, kwa njia zipi? Kama sivyo, inatofautianaje?

  • Wanafamilia wanafanya nini? Je, watu katika familia yenu wanaweza kuwa na mwenendo kama huo?

  • Unafikiri mwandishi anataka watu waamini nini kuhusu familia?

Mfano B: Hadithi iliyotayarishwa shuleni

Unaweza kuuliza maswali kama:

  • Shule katika hadithi inafanana na shule yetu?

  • Ni kwa njia zipi majengo yanafanana? Ni kwa njia majengo ni tofauti?

  • Ni kwa njia zipi watu - mwalimu mkuu, walimu, wanafunzi - wanafanana na wale wa shuleni kwetu? Ni kwa njia zipi wanatofautiana?

  • Je, watu katika hadithi wana mwenendo au wana matendo kama watu wa shuleni kwetu au wana mwenendo au wanatenda tofauti? Toa mifano kuthibitisha jibu lako.

  • Unafikiri mwandishi katika hadithi anawataka wasomaji kuamini nini kuhusu shule?

Angalizo: Unaweza kuuliza maswali kama haya kuhusu kijiji, mji, jiji ambapo hadithi kama hii inatolewa. Lengo ni kuwafanya wanafunzi kulinganisha kati ya yale wanayoyajua na wanayosoma juu yake.

Nyenzo-rejea ya 2: Vidokezo vya barua ya mwandishi