Somo la 1

Ujuzi wa hadithi kwa wanajumuia ni nyenzo muhimu katika mazoezi ya kusikiliza na kuzungumza nje na ndani ya darasa. Ni muhimu wanafunzi wajifunze kuheshimu na kupenda busara na urithi wa lugha zao za nyumbani na tamaduni zao. Kwa kuimarisha stadi zao za kuzungumza na kusikiliza lugha za nyumbani kwa njia inayofurahisha, wanafunzi watakua katika hali ya kujiamini pia.

Kwa kuwa sanaa ya kusimulia hadithi haipewi thamani katika baadhi ya jumuia, watu wanaweza kuwa wamesahau baadhi ya tondoti na thamani za hadithi. Njia ya kujenga Nyenzo-rejea lugha kwa wanafunzi wako ni kuweka wazi matoleo ya zamani na halisi ya hadithi. Unaweza kufanikisha jambo hili kwa kuzungumza na watu wengine katika jumuia.

Uchunguzi kifani ya 1: Matumizi ya lugha nyingi za wanafunzi wako darasani

Bwana Kimaryo hufundisha darasa la 4 katika shule ya msingi Makanya iliyopo nchini Tanzania. Shule ipo karibu na shamba la mkonge, ambapo wafanyakazi huzungumza lugha nyingi mbalimbali. Katika darasa lake lenye wanafunzi 70, wanafunzi 10 wanazungumza Kichaga, wanafunzi 6 wanazungumza Kirundi, wanafunzi 3wanazungumza Kinamwanga na waliobakia wanazungumza Kipare. Kwa kawaida yeye huzungumza Kiswahili anapowafundisha

Bwana Kimaryo aliwataka wanafunzi wake kukusanya hadithi toka majumbani mwao na kuwajengea hali ya kujiamini katika kuzungumza kwa kusimulia hadithi kwa kutumia lugha zao za nyumbani. Alianza somo lake kwa kuwaonesha wanafunzi picha ya mtu wa makamo na baadhi ya wanafamilia waliokuwa wamekaa pembezoni mwa moto. Kisha akawataka wanafunzi wawili wawili kujadili watu hawa wanafanya nini. Vikundi viliwasilisha majibu yao darasani. Kisha akawauliza wanafunzi kama na wao hukaa pembezoni mwa moto na kusikiliza hadithi, wengi waowalisema hawafanyi hivyo. Aliwataka wanafunzi waende nyumbani na kumuomba mtu mmoja wa makamo awasimulie hadithi.

Katika somo lililofuata, aliwaganya wanafunzi katika vikundi. Aliunda vikundi viwili vya wazungumzaji wa Kichaga, kikundi kimoja cha wazungumzaji wa Kirundi, na kikundi kimoja cha wazungumzaji wa Kinamwanga. Aliwagawanya wazungumzaji wa Kipare katika vikundi kumi. Akamtaka kila mwanafunzi asimulie hadithi yake kwa wanakikundi wenzake kwa kutumia lugha ya nyumbani.

Bwana Kimaryo alizunguka katika vikundi na kusikiliza namna wanafunzi walivyokuwa wakisimulia hadithi. Alifurahia sana namna walivyokuwa wakisimulia hadithi, hususani namna walivyokuwa wakitumia sauti zao kuongeza mvuto.

Shughuli ya 1: Kusimuliana hadithi kwa kutumia lugha za nyumbani

Katika sehemu ya 1,wanafunzi wako wameshabaini mbinu muafaka ya kusimulia hadithi toka kwa wazee wao. Huu sasa ni wakati muafaka kwa wao kukusanya hadithi toka kwao.

Zungumza na wanafunzi wako kuhusiana na uzoefu wao katika kusikiliza hadithi na kubaini ni aina gani ya hadithi wanazozifurahia. Waulize kama wanasikiliza hadithi nyumbani na akina nani husimulia hadithi katika jumuia zao.

Waagize wamtafute mtu mmoja toka katika jumuia zao za nyumbani ili awasimulie hadithi. Watatakiwa kuwa na kumbukumbu za hadithi hizi, kwa sababu watahitajika kuwasimulia wenzao darasani. Njia nzuri ya kujifunza hadithi ni kwa wao kuwasimulia watu mbalimbali nyumbani. Kadiri watakavyokuwa wanafanya hivi, watatakiwa kuzingatia kuwa wana taarifa zote muhimu za hadithi.

Katika somo lijalo, waweke pamoja wanafunzi wenye lugha za nyumbani zinazofana (tazama Nyenzo-rejea muhimu: Tumia kazi ya kikundi katika darasa lako). Waagize wasimuliane hadithi walizokusanya kwa kutumia lugha zao za asili.

Je wanafunzi wako wamepokea vipi shughuli hii?

Je unaweza vipi kujenga utashi katika hadithi hizi?

Sehemu ya 2: Njia za kukusanya na kutenda hadithi