Somo la 1

Ukiwa mwalimu, utatoa maelekezo ya aina mbalimbali kwa wanafunzi wako.

Unaweza kutumia maelekezo ya kila siku kukuza msamiati mpya na stadi ya usikilizaji katika lugha ya ziada. Maelekezo hutumia muundo wa amri wa kitenzi. Wakiona muundo wa kuamuru katika kitenzi mara kwa mara katika mazingira yanayoleta maana, wanafunzi wataanza kuelewa na kujifunza muundo huo.

Wanafunzi wanapojifunza lugha mpya, usikilizaji huendelea haraka kuliko mazungumzo. Wanahitaji nafasi kubwa ya kusikiliza na kujibu katika lugha mpya. Katika hatua za mwanzo za ujifunzaji lugha (na baadaye pia), unaweza kutumia shughuli ambazo zinawahitaji kujibu kwa vitendo lakini haiwahitaji kujibu (kwa maneno) hadi wanapojisikia kuwa na uhakika zaidi. (Hii mara nyingi huitwa ‘mawazo ya mbinu jumuishi’- Angalia Nyenzo-rejea 1: Mawazo ya mbinu jumuishi .)

Uchunguzi kifani ya 1: Uongozaji wa darasa katika Kiingereza

Bibi Mujawayo anafundisha darasa la kwanza mjini Kigali, Rwanda. Anatumia Kiingereza katika uendeshaji wa darasa.

Asubuhi husalimiana na wanafunzi katika lugha zao za nyumbani, na huwauliza habari zao za nyumbani katika lugha zao.

Baada ya baraza, huanza kutumia Kiingereza darasani, ‘Pangeni mstari wanafunzi’ na huwaelekeza barazani, mahali ambapo wanapaswa kujipanga. ‘Ingia darasani’ husema huku akiwaonesha vitendo vya kuwaelekeza kuingia ndani. ‘Simameni karibu na madawati yenu.

Mwalimu na wanafunzi husalimiana kwa kutumia Kiingereza. Husema ‘Kaeni chini.

Hurejea tena katika lugha yao ya nyumbani ili kuanza kusimulia hadithi hadi anapowaweka katika vikundi, kwa ajili ya shughuli mbalimbali.

Kila kikundi kina alfabeti. Husema kwa Kiingereza kwa kunyoosha mikono A na B nyosheni mikono. Kwa kuonesha katika kisanduku huwaambia ‘Chukueni vitabu kutoka katika kisanduku.’ ‘Kaa chini, na msomee mwenzio.’ Kama wanaonekana kutoelewa, wanaigiza wanachopaswa kufanya.

Baadaye hutoa maelekezo zaidi kwa Kiingereza, bila kutafsiri. Vikundi viwili vinapaswa kuonesha hadithi yao na kikundi kingine watasoma pamoja naye katika lugha yao ya nyumbani kutoka katika kitabu kikubwa.

Bibi Mujawayo anagundua kuwa wanafunzi wake wanaanza kuelewa haraka maelekezo katika Kiingereza, na mara huanza kusema maneno.

Shughuli ya 1: Simple Simon husema

Katika mchezo huu unaojulikana sana, wanafunzi hufuata kwa vitendo maelekezo. Unaweza kutumia njia hii kuongeza msamiati na stadi ya usikilizaji katika maeneo mbalimbali ya masomo.

Kiongozi hutoa amri na kuonesha vitendo wakati huohuo. Wanafunzi wanapaswa kufuata amri hiyo kutoka kwa Simple Simon. (Unaweza kubadilisha jina hili kwa kutumia jina la mtu ambaye ni mashuhuri kijijini.) Mchezo huchezwa kama hivi:

Kiongozi: Simple Simon anasema , ‘Ruka!’ (Kiongozi anaruka.)

Wanafunzi wanaruka.

Kiongozi: Simple Simon husema, ‘Shika vidole vya miguu !’ (Kiongozi anashika vidole vya miguu)

Wanafunzi wanashika vidole vya miguu.

Kiongozi: ‘Kuna pua yako!’ (Kiongozi anakuna pua yake.)

Baadhi hukuna pua zao. Wengine hawafanyi hivyo. Wale ambao wamekuna pua zao wanatoka (kwa sababu amri haikutoka kwa Simple Simon Na kuendelea hivyo….. Tumia maelekezo rahisi kwa wanafunzi wanaojifunza lugha ngeni, maelekezo magumu kwa wale ambao ni wanaielewa lugha zaidi. Anza polepole, lakini endelea kwa kasi zaidi. Mshindi ni yule aliyebaki.

Sehemu ya 1: Kuandaa mazingira asilia kwa ajili ya mazoezi ya lugha