Somo la 2

Ni jambo muhimu kuwapa wanafunzi nafasi ya asilia ya kuendeleleza stadi zao katika lugha ya ziada. Hapa tunapendekeza njia ambazo unaweza kuzitumia kushirikisha jamii na kutumia stadi za asilia na busara kama njia ya Nyenzo-rejea ya shughuli za darasani.

Umeona, katika Uchunguzi-kifani 1 na shughuli 1, namna maelekezo ya kila siku yanavyoweza kuleta muktadha asilia wa ujifunzaji lugha. Wanafunzi walisikiliza na kuonesha uelewa kwa vitendo. Katika sehemu hii tunashauri utumie mapishi ya asilia na mchakato kama njia ya muktadha wa mafunzo, ukiwapa nafasi wanafunzi kuzungumza (na kuandika) na vilevile kusikiliza.

Shughuli zilizotumika hapa zitaendelezwa mbele katika sehemu ya 5, ambapo darasa lako litaanza kutayarisha kitabu cha mapishi.

Uchunguzi kifani ya 2: Wanafunzi watu wazima hujifunza kwa vitendo

Baadhi ya wanafunzi wa Kiswahili walitumia muda wa siku nzima mjini kama sehemu ya kozi yao. Kila mwanafunzi alikuwa akifuatana na msaidizi wa lugha ambaye alikuwa mzungumzaji wa Kiswahili. Wasaidizi waliwasaidia wanafunzi walipokuwa wakijaribu lugha waliojifunza; wakinunua mboga kutoka kwa wauzaji wa barabarani na kuzungumza na familia zilizokuwa zinawasaidia.

Sehemu muhimu ya siku hiyo ilitumika kupika chakula. Mwanafunzi alipaswa kupika chakula, akielekezwa na msaidizi wa lugha. Upikaji ulikuwa umefanyiwa mazoezi na kuigizwa, na mara nyingi kuandikwa au kurekodiwa katika kinasa sauti, wiki moja kabla darasani. Wanaume walipewa maelekezo ya kutayarisha moto, wakati wanawake walitakiwa kupika chakula kama ugali, ndizi na nyama na kabichi. Walizungumzia pia jinsi ya kubadilishana nafasi ili kuwasaidia kujifunza lugha.

Wakati chakula kilipokuwa tayari, nyimbo za Kiswahili ziliimbwa, na wanafunzi walijifunza michezo ya asili ya Kiswahili ya watoto. Baada ya vyombo kusafishwa, kundi la wanafunzi wenye furaha na uchovu walijipakia katika teksi na kurudi nyumbani.

Shughuli ya 2: Kujifunza kwa vitendo vya shughuli za kijamii

Waambie wanafunzi wako kwamba watakwenda kutafuta jinsi shughuli za nyumbani zinavyotekelezwa na kueleza njia za mchakato katika lugha ya ziada. Watake wanafunzi kuleta taarifa kutoka nyumbani au mkaribishe mwenyeji shuleni kutoka katika jamii ili kuonesha stadi.

Wagawane wanafunzi katika jozi au katika vikundi (vikundi hivi vinaweza kuwa vya mchanganyiko wa uwezo tofauti), kufanya kazi, na ikiwezekana kuandika hatua za moja ya mchakato katika lugha ya ziada. Zungukia darasa na kuwasaidia msamiati mpya ambao watuhitaji.

Vipe vikundi muda wa kukariri na kufanya mazoezi ya hatua zinazotumika, katika kujitayarisha kuwasaidia wengine. Wanaweza kukusanya toka nyumbani vitu vinavyohitaji katika mchakato huo.

Siku inayofuata, mpe nafasi mwanafunzi mmoja kutumia lugha ya ziada kuelekeza mjumbe wa kikundi kingine, wakati huohuo darasa likiangalia k.m. kusafisha nyumba.

Wanafunzi wamefanyaje katika shughuli hiyo?

Unaweza kuitumia njia hiyo katika mchakato mwingine ili kukuza msamiati wao?

Kama jibu ni ndiyo, vipi?