Nyenzo-rejea ya 1: Mjumuisho wa mwitikio wa vitendo

Usuli/taarifa ya mwanzo/uelewa wa mwalimu

Kwa toleo la mtandaoni:

http://www.tpr-world.com/ [Tip: hold Ctrl and click a link to open it in a new tab. (Hide tip)]

Webu inatoa taarifa kuhusu mjumuisho wa mwitikio wa vitendo kama njia ya kufanya kazi katika ujifunzaji lugha. Kuna maelezo mengine ambayo unaweza kufuatilia.

Kwa ajili ya kuhariri matini

Unaweza kuwajulisha wanafunzi wako muundo wa lugha mbalimbali kutokana na vitendo vya kimchezo ambavyo vinawahitaji kufuata maelekezo kwa vitendo (mjumuisho wa mwitiko wa vitendo). Hapa kuna mifano ya namna ya maelekezo ambayo unaweza kuwapa wanafunzi. Weka mkazo katika aina moja ya maelekezo kwa wakati mmoja, ili wanafunzi waelewe jinsi lugha inavyofanya kazi

Mtingishiko wa mwili

Simama.

Cheka.

Kohoa.

Lia.

Gonga meza.

Vitendo na vifaa

Onesha mlango.

Okota kalamu.

Funga dirisha.

Nusa ua.

Onesha mlima.

Onesha mwanamke anayetengeneza keki.

Vitendo, vifaa na watu

Chukua kalamu na umpe Nuru

Tafuta kitabu na unipe

Okota karatasi na mpe Thimba.

Ongeza vimilikishi

Mpe Aida kitabu cha Thimba.

Leta peni ya Nuru kwangu

Mpe Kito kitabu chake.

Mpe Eshe miwani yake.

Hiki na kile; hapa na pale

Mpe hiki Adia.

Tafuta kile kutoka kwake.

Tafuta kalamu na iweke hapa.

Tafuta kitabu na kiweke pale.

Kuhusisha nafasi

Weka kalamu katikati ya vitabu viwili.

Weka kalamu karibu na rula.

Weka kifutio ndani ya kisanduku.

Weka rula juu ya kisanduku.

Jumlisha namba, ziweke rangi na ukubwa

Weka kalamu mbili ndani ya kisanduku.

Chukua mawe matatu nje ya kisanduku.

Okota kalamu nyekundu na mpe Thimba.

Weka kitabu cha kijani mezani.

Chukua kitabu kidogo na mpe Nuru.

Weka kitabu kikubwa ndani ya kisanduku.

Maelekezo na maelezo, pamoja mazungumzo kiasi

Fanya na kusikiliza

Wanafunzi wanafanya tendo. Mwalimu (au mwanafunzi mwingine) husema wanachofanya (k.m. ‘Umesimama.’)

Sikiliza na kufanya

Mwalimu (au mwanafunzi mwingine) anamuelekeza mwanafunzi (k.m. Simama.’ Mwanafunzi anafuata amri, kwa kufanya tendo.

Sahihi au si sahihi

Mwanafunzi anajifunza kusema ‘sahihi’ na ‘si sahihi’. Mwalimu (au mwanafunzi mwingine) anatenda tendo, na kutoa tamko ‘lililo sahihi’ au ‘lisilo sahihi’ kuhusu anachofanya (k.m. ‘Nimekaa.’) Wanafunzi wanasema ‘kweli’ au ‘si kweli’

Sikiliza, igiza na tenda

Mwalimu (au mwanafunzi mwingine)anamuelekeza mwanafunzi. Mwanafunzi anarudia yaliyosemwa na halafu anatenda amri hiyo.

Eleza, sikiliza na igiza

Mwanafunzi hutenda na kueleza wanachofanya (k.m. ‘Nimesimama.’) Mwalimu ( au mwanafunzi mwingine) anaeleza kile kilichosemwa na mwanafunzi na anatekeleza kitendo.

Kwenda nje au kutumia picha ili kuongeza msamiati

Mwanzoni, unahitaji kutumia maneno yanayojulikana na maelekezo mapya. Baada ya msamiati wa darasa kujulikana, unaweza kutumia msamiati wa nje ya darasa, k.m.:

Gusa jani.

Onesha mbingu.

Unaweza pia kuongeza msamiati kwa kutengeneza kadi zenye maneno au picha, k.m. picha za aina ya chakula:

Chukua nyama na mpe Nuru.

Tafuta mkate wa Kapuki na unipe.

Zimetolewa kutoka: Total Phsyical Response Worldwide, Website

Nyenzo-rejea 2: Mapishi