Sehemu ya 2: Njia zijengazo ufasaha na usahihi

Swali Lengwa muhimu: Unawezaje kuwasaidia wanafunzi kujenga hali ya kujiamini katika utumiaji wa miundo ya lugha mahsusi?

Maneno muhimu: vitenzi; vielezi; urudiaji; mashairi; nyimbo; uhariri

Matokeo ya ujifunzaji

Mwishoni mwa sehemu hii, utakuwa umeweza:

  • umewaongoza wanafunzi wako katika kuwapa ujuzi wa kudhibiti miundo ya lugha ya ziada;
  • umetumia urudiaji, nyimbo, mashairi na hadithi katika kufundisha miundo ya lugha;
  • umewasaidia wanafunzi wako kusimamia kazi yao wenyewe kadri wanavyotafuta maana na matumizi sahihi ya vitenzi.

Utangulizi

Ukiwa mwalimu wa lugha ya ziada, mara zote unatakiwa utafute mbinu mpya za kuwapa wanafunzi wako uzoefu wa lugha hiyo. Kama wanapewa fursa za kujizoeza lugha hiyo, matumizi yao ya lugha hiyo yatakuwa fasaha na sahihi zaidi.

Sehemu hii inakupatia mazoezi yanayofaa ambayo yanalenga katika kauli na miundo mahsusi.

Kumbuka kwamba vitendo utakavyovichagua ni lazima viwe vinafahamika kwa wanafunzi, ama kitendo chenyewe, au katika maisha yao (inapendelewa viwe vinavyohusu sehemu zote mbili).

Nyenzo-rejea 2: Mapishi