Nyenzo-rejea 4: Shairi la kusifu

Kwa matumizi ya wanafunzi

Ngoma Yangu na Francis Faller

Inapiga

kwa uvumilivu

kama maji

yadondokayo

toka kwenye

bomba la

mfereji

au kwa majivuno

kama sauti ya mapigo ya maji ya bahari.

Ngoma yangu. Ngoma yangu.

Inaita upendo.

Inatwanga hasira.

Inahubiri uhuru.

Haisimami kamwe

Hata wakati hakuna mtu

anayesikia ngoma yangu

isipokuwa mimi.

Ngoma yangu inasalimia

kila kitu

kipitacho njia:

jua linalochomoza

mvua inayogongagonga

upepo unaovuma

familia ya korongo

makazi pote angani.

Inamsalimia chenene

Anayelia mlio mwembamba kwa sababu ya raha yake.

Inawasalimia wafanyakazi

ambao vifaa vyao vya kutobolea na kupasulia

vinachimba mashimo

kwa kuchosha.

Ninaifuatilia

katika kicheko

Ninaiongoza kuvuka

maumivu yanayopwita.

Ni shorewanda anayedonoa mbegu

ni ufito kando ya ukingo

ni risasi iendayo kasi.

Ngoma yangu. Ngoma yangu.

Inapiga kwa kiherehere

makaribisho

kwa ajili yako.

Je, utaisikia

kwa furaha?

Je, utakimbia kwa hofu?

Ngoma ni

ngozi na mbao tu

kwa hiyo utakuja?

Ni lazima uje.

Ni lazima uje.

Ngoma yangu kipenzi

ilikuwa jana dhaifu sana.

Leo inapiga.

Kwa nguvu.

Hakika haikutumika zaidi

duniani kote

kupiga bure.

Ingawa kamwe

haipati jibu

Nafikiri

sitaweza kuishi

kama wimbo

wa ngoma yangu

utakufa.

Chanzo asilia: My Drum – Meyerowitz, B., Copans, J. & Welch, T. (watunzi)

Nyenzo-rejea 3: Chati za njeo za kitenzi

Nyenzo-rejea 5: Vitenzi na vielezi katika shairi – Ngoma Yangu na Francis Faller