Somo la 2

Ukiwa mwalimu, mara zote unapawa kutafuta shughuli ambazo zinakuza ujuzi wa kusikiliza kwa kuelewa.

Hapa, Shughuli 2 inahusisha kusikiliza na kuchora, au kubadili lugha ya taarifa kwenda katika kielelezo cha taarifa. Ina faida inayofanana na mwitikio wa mwili wote (total physical response); kwa sababu wanafunzi hawalazimiki kutumia lugha katika kuonesha welewa wao. Hata hivyo, inatakiwa yule anayeelezea awe fasaha na sahihi sana –vinginevyo, athari zinaweza kuonekana kwenye picha ya mwanafunzi mwenza.

Uchunguzi kifani ya 2: Kueleza na kupanga mawasiliano yasiyofahamika kwa njia ya posta

Aghalabu, Lulu alikuwa akipata ‘mawasiliano asiyoyafahamu’ yaliyowekwa kwenye sanduku lake la barua: matangazo kutoka kwenye maduka mbalimbali yanayoonesha picha za bidhaa zao. Siku moja aliamua kuyaweka, badala ya kuyatupa kwenye pipa la taka.

Alikata sehemu tofauti tofauti za bidhaa za nyumbani: pakiti za vyakula, sukari na unga; maboksi ya sabuni za unga na nafaka, nk. Alikuwa na nakala nyingi.

Alichora picha sita za vinafasi vya kabati la jikoni, na kuchomeka bidhaa za nyumbani katika vijinafasi vitatu ( Nyenzo-rejea 4: Eleza na panga sinaonesha mifano). Kila moja kati ya picha hizo tatu ilikuwa tofauti na nyingine. Kisha alikata nakala za bidhaa zote kwenye vijinafasi vya kabati la jikoni. Bado alibakiwa na vijinafasi titatu visivyo na kitu.

Siku iliyofuata, kwenye Darasa lake la 4, makundi matatu ya wanafunzi sita sita au saba saba yalipewa picha za vijinafasi vya kabati vilivyojaa vitu. Vile

vilivyokuwa vitupu, viligawiwa kwa makundi mengine matatu, na wanafunzi tofauti katika makundi haya walipata nakala za bidhaa.

Aligawa makundi hayo katika sehemu mbili, na kulifanya sehemu ya 1 (ililo na picha zilizokamilika) kukaa karibu na sehemu ya 2 (yenye vijinafasi visivyo na kitu na bidhaa tofauti). Wanakundi la sehemu 1 walieleza jinsi bidhaa zilivyopangwa kwenye vijinafasi, na wanakundi la sehemu 2 walizipanga katika vijinafasi vilivyokuwa vitupu. Waliuliza maswali pale ambako hawakuwa na uhakika. Mchezo huu uliwapa zoezi la kutumia maneno kuhusu nafasi mbalimbali katika mazingira ‘halisi’.

Somo lilikwenda vizuri. Lulu aliamua kwamba wakati mwingine atakuza msamiati wa wanafunzi wake kwa kuwaambia wachambue na kueleza taswira za –au, kama itawezekana, ngoma-halisi na vitu vilivyobuniwa kutoka katika jumuiya ya mahali hapo.

Shughuli ya 2: Eleza na chora

Shughuli hii hufanywa katika makundi au na watu wawili wawili. Mtu mmoja anaeleza na mwingine/wengine anachora/wanachora. Darasa lenye wanafunzi wa viwango mbalimbali, wanafunzi wakubwa wanaweza kutoa maelezo, na wadogo wachore.

Tafuta picha au michoro rahisi sana au chora ya kwako, m.f. mchoro wa vistari wa picha ya nyumba au mti. Utahitaji picha moja kwa kila jozi au kundi la wanafunzi. Picha zinaweza kuwa sawasawa au tofauti.

Anza kuwafundisha wanafunzi msamiati na aina za sentensi ambazo watahitaji kuzitumia, mfano, ‘Chora mraba katikati ya ukurasa’. ‘Chora kuku wawili kando ya nyumba.’

Toa picha moja kwa kila jozi (au kundi) la wanafunzi, huku ukiwaambia ‘watoa maelezo’ kutowaonesha wenzao picha hizo. Mwanafunzi aliyeshika picha anaielezea picha hiyo kwa wanafunzi wengine/mwanafunzi mwingine, ambaye anajaribu kuchora kitu kinachotolewa maelezo. Hawatakiwi kusema picha hiyo ni nini.

Mwishoni, mtoa maelezo na mchoraji wanalinganisha picha zao. Anza mjadala wa darasa zima: Duara la ‘Asanda’ ni dogo kuliko lililoko katika picha’. Kuku wa Amina wana vichwa vikubwa, lakini kuku walioko katika picha wana vichwa vidogo.’ Wakiwa wanafanya mazoezi, wataifanya vizuri zaidi shughuli ya aina hii.

Nyenzo-rejea Muhimu: Kufanya kazi katika madarasa makubwa/madarasa ya mchanganyiko kunatoa mawazo zaidi kuhusu mbinu za kufanya kazi.