Somo la 3

Ukiwa mwalimu, unapaswa kukumbuka kwamba aghalabu, binadamu (pamoja na wanafunzi) hutaka kujua maana ya kitu wanachokifanya. Kila shughuli unayowapa wanafunzi lazima iwape fursa ya kutafuta maana.

Uchunguzi-kifani 3 na Shughuli Muhimu vinatalii njia za kutafuta maana katika aya au matini. Wanafunzi wafanye mazoezi ya baadhi ya maarifa muhimu yaliyomo katika maandishi hayo: utabiri na utazamiaji (kukisia kitu gani kitatokea baadaye). Walitakiwa pia kuwasiliana miongoni mwao ili kutatua tatizo. Kila mmoja alikuwa na nafasi ya kuchangia ili kutatua ‘fumbo’ na kutafuta maana.

Uchunguzi kifani ya 3: Hadithi: kutoka vyanzo tofauti na kuwekwa pamoja

Darasa la 6 la Bibi Ndaba lilileta hadithi kutoka majumbani na kuzieleza kwa ufafazi. Katika kila ukurasa, waliandika sentensi na kuchora picha inayoona na sentensi husika. Kurasa hizo zilipachikwa kwenye magamba ya plastiki ya kurekodia na kuunda jarida ambalo ili kutengeneza kitabu.

Mfanyakazi mwenzie, Bibi Mapande, ambaye anafundisha darasa la 3 aliziona hadithi zilizofafanuliwa, na akaomba kuziazima kwa ajili ya shughuli ya kusoma katika darasa lake. Bibi Ndaba alifika kuangalia darasa la mwenzie.

Bibi Mapande aliligawa darasa lake katika makundi matano. Alilipa kila kundi hadithi lakini alizitoa kurasa kutoka kwenye jarida na kuliweka jarida hilo katikati ya meza. Alimpa kila mwanafunzi katika kundi ukurasa mmoja wa hadithi, huku akihakikisha kwamba amechanganya mpangilio wa kurasa hizo. Kila mwanafunzi alitakiwa kusoma sentensi iliyo kwenye ukurasa wake mbele ya kundi lake. Kwa njia ya majadiliano, kundi liliamua sentensi ipi ikae mwanzo wa hadithi, na kuweka sentensi nyingine zote katika mpangilio unaostahili; na kurudishia kurasa katika jarida kwa mpangilio sahihi.

Bibi Mapande alimwambia mwanafunzi mmoja kutoka katika kila kundi, asome hadithi ya kundi lake mbele ya darasa; na wanadarasa walitoa maoni kuhusu mpangilio wa sentensi. Wakiwa katika darasa, walichagua hadithi waliyoipendelea zaidi, na igizo la dakika tano likaandaliwa kuonesha hadithi hiyo.

Shughuli muhimu: Sehemu za kitu kizima

Unaweza kutumia shughuli ya aina hii kwa darasa la kiwango chochote

Chagua hadithi fupi, iliyoandikwa vizuri, au aya ambayo wanafunzi wako wanaweza kuielewa na kuihusisha na ukweli. Unaweza kutumia hadithi, hadithi au aya za/ya picha kama zile zilizoko katika Nyenzo-rejea: Kuunda maana , au aya ambayo ni changamano zaidi ya lugha au mada yoyote. Kila kundi linaweza kuwa na hadithi hiyo hiyo au tofauti ya kushughulikia.

Ikate hadithi katika vipande sita au saba. Vipande vyaweza kuwa aya, sentensi au kundi la sentensi, kulingana na umri na uwezo wa wanafunzi wako. Pachika kila kipande kwenye kadi.

Lipe kila kundi seti ya sehemu za aya zilizokatwa.

Kila mwanakikundi ana kipande cha aya, na anawasomea wengine kipande chake. Wakiwa kama kundi, wanaziweka aya zao pamoja katika mpangilio wake sahihi.

Kwa wanafunzi ambao wana uwezo au uzoefu zaidi, waambie waeleze jinsi walivyofanya mpaka kupata mpangilio sahihi.

Soma aya au hadithi hizo mbele ya darasa.

Nyenzo-rejea ya 1: Shughuli zaidi zihusuzo tofauti za taarifa