Nyenzo-rejea ya 1: Shughuli zaidi zihusuzo tofauti za taarifa

Nyenzo za mwalimu kwa ajili ya kupanga na kutumia na wanafunzi

Kufanana ni nini?

Chagua seti za picha sita au nane. Kila seti ya picha lazima iwe na kitu kinachofanana kwa picha zote. Kwa mfano, unaweza kuwa na picha sita ambazo zote zina kitu kimoja ambacho kimetengenezwa kwa kioo, au seti ya picha sita ambazo katika kila picha kuna mtu anakula. Pengine una picha sita ambazo zinaonesha mtoto, au zinaonesha umaskini, au ukarimu.

Gawa darasa lako katika makundi ili kila kundi linaweza kuwa na seti ya picha kadhaa. Hakikisha kwamba una baadhi ya picha za akiba, kwa ajili ya kundi lolote litakalomaliza kazi haraka. Mara kundi linapomaliza, unaweza kukusanya seti za picha zao na kuzigawa kwa kundi lingine ambalo limemaliza.

Wanakikundi wasioneshane picha zao. Wanatakiwa kuulizana na watu wengine katika kundi aina ifuatayo ya maswali:

Je, kuna (kitu)…. katika picha yako?

Je, kuna (vitu)…. katika picha yako?

Je, picha yako inaonesha …. ?

Wanakikundi wengine wanajibu:

Hapana, hakuna. Au, Ndiyo, ipo/zipo.

Hapana, haioneshi. Au, Ndiyo, inaonesha.

Mtu ambaye anabainisha sifa ya ufanano ndiye mshindi.

Mchezo huu ni rahisi au mgumu zaidi kutegemeana na kiwango cha udhahania kilichomo kwenye sifa ya ufanano.

Unafanya nini ili kujipatia kipato?

Andika orodha ya kazi ubaoni, kama hii iliyopo hapa chini.

DaktariDaktari wa MenoMwalimu
Muuza dukaMuuguziMeneja
KaraniRubaniMhandisi
Mtunza BustaniMkutubiAskari polisi
MkulimaMchuuzi wa samakiFundi wa ngamizi
Mhudumu katika ndegeMfamasiaMama Ntilie/Lishe
Mtaalam wa mauaMwanasayansiMwanamuziki
Mtaalam wa ngamiziMhudumu wa dukaniFundi gereji

Waambie wanafunzi waseme wangependa kufanya nini watakapomaliza masomo yao. Wanaweza kuongeza kazi nyingine katika hizo zilizoorodheshwa.

Toa kadi kwa jozi za wanafunzi na waambie waandike jina la kazi kwenye kadi hiyo. Kwenye kadi nyingine, wanatakiwa waandike fasili ya kazi hiyo.

Mwambie mwanafunzi mmoja kutoka katika kila jozi kutoa ripoti mbele ya darasa kuhusu kazi waliyonayo, na fasili yake. Wanafunzi wengine lazima watoe maoni kama wanadhani fasili ni sahihi.

Kusanya kadi za kazi na maana zake, zisambaze kwa wanafunzi bila kufuata utaratibu wowote. Waambie wanafunzi wazunguke darasani na kutafuta mwenza ambaye ana fasili au neno sahihi.

Wenza wanapopatana, wanatakiwa wasimame pamoja mpaka kila mmoja hapo darasani amalize shughuli hiyo.

Kisha waambie waunde sentensi kwa kutumia kazi walizozifasili.

Nyenzo-rejea 2: Madokezo kwa ajili ya picha