Somo la 3

Baada ya stadi na welewa kuimarishwa katika lugha inayofahamika vizuri, ni rahisi zaidi kuvihamishia kwenye lugh aya ziada. Wataalamu wengi huamini pia kuwa kama mtu ataliangalia somo kutumia mitazamo ya lugha mbili, stadi zao za kufikiri huwa bora. Ni muhimu uhakikishe wanafunzi wako wanajiona kuwa tajiri –badala ya fukara –kwa kuwa na lugha mbili au zaidi.

Wanafunzi wako wanapojadili mawazo katika lugha ya nyumbani au lugha ya mawasiliano mapana, inafaa kutafuta and kujifunza njia za kueleza mawazo haya katika lugha ya ziada. Unapaswa daima kufikiria njia kuwasaidia kufanikisha hili. Kisehemu hiki kinakupatia mawazo kadhaa.

Uchunguzi kifani ya 3: Kueleza mawazo kwa Kiingereza

Zawadi alihakikisha kuwa tini katika Kiswahili juu ya somo la mfalme namshona-viatu hazikufutwa ubaoni.

Katika somo lililofuata la darasa la 7, alianza kujadiliana na wanafunzi jinsi ya kujibu, kwa Kiingereza, maswali aliyokuwa ameuliza.

Walizungumzia baadhi ya maneno au mafungu muhimu waliyokuwa wametumia, mathalani tabia, maumbile. Ni mtu au sifa ya namna gani iliyorejelewa na kila neno? Walifahamu watu wenye sifa hizo?

Walijadili pia, kwa njia hiyo hiyo, baadhi ya maneno muhimu ya Kiingereza katika maswali: educated (mwenye elimu); wise (mwenye busara); clever (mjanja); happy (mwenye furaha); learned (msomi). Aliwakumbusha kuwa hakuna tafsiri sisisi wakati wote kutoka Kiingereza kwenda Kiswahili au kutoka Kiswahili kwenda Kiingereza. Hata hivyo walipata njia za kueleza mawazo yaliyokuwa ubaoni kwa Kiingereza. Katika kufanya hivyo, walijifunza miundo mipya ya lugha na msamiati mpya.

Zawadi aliyaandika haya ubaoni, na akawataka wafanye kazi katika vikundi na kuandika majibu ya maswali yake mawili kwa Kiingereza. Kikundi kingeweza kuandaa majibu pamoja, lakini kila mwanafunzi alipaswa kuandika majibu yake mwenyewe.

Zawadi aligundua kuwa mbinu ya kubadili msimbo iliwasaidia wanafunzi wake kukuza Kiingereza chao zaidi.

Shughuli muhimu: Mtu mzima ambaye ningetaka niwe: Kauli ya Dira

Watake baadhi ya wanafunzi wako kuwasilisha maelezo ya watu wazima wanaowaheshimu darasani. Litake darasa kubainisha watu wazima wawili wanaowaheshimu katika jumuiya yao, na panga ili watu wazima hawa wazungumze na wanafunzi.

Amua kuhusu maswali ya kuuliza, k.m.:

Ni jambo lipi ni muhimu kabisa katika maisha?

Ni tajiriba zipi za maisha zilizokufanya uwe imara zaidi?

Nani aliyekuwa na athari kubwa kabisa kwako katika makuzi yako?

Kubalianeni nani atauliza maswali, na jinsi ya kurekodi yanayosemwa. Wanafunzi na watu wazima yumkini watatumia lugh aya nyumbani.

Baada ya ugeni, jadilianeni wanafunzi walichojifunza.

Waulize wanafunzi: Ni sifa na maadili yapi ungependa kuyajenga ili uwe nayo ukiwa mtu mzima?

Tafuta maneno ya lugha ya nyumbani na lugha ziada yanayotaja sifa na maadili haya, na uyaandike.

Watake waandike kauli za dira na/au malengo yao katika lugha ya ziada. ( Nyenzo-rejea 5: Kauli za dira na lengo inatoa mifano.)

Nyenzo-rejea ya 1: Shairi