Nyenzo-rejea ya 1: Shairi

Nyenzo za mwalimu kwa ajili ya kupanga na kutumia na wanafunzi

Wewe!

Kichwa chako ni kama ngoma tupu.

Wewe!

Macho yako ni kama mabonge ya moto.

Wewe!

Masikio yako ni kama pepeo za kuchochea moto.

Wewe!

Tundu la pua yako ni kama shimo la panya.

Wewe!

Mdomo wako ni kama bonge la tope.

Wewe!

Mikono yako ni kama mikwiro.

Wewe!

Tumbo lako ni kama chungu cha maji machafu.

Wewe!

Miguu yako ni kama nguzo za miti.

Wewe!

Mgongo wako ni kama kilele cha mlima.

Ibo

Tini za Mwalimu

Shairi hili limeundwa kwa mfuatano wa tashibiha. (Katika mfano huu, mfuatano wa tashibiha ni mfuatano wa matusi pia!). Tashibiha ni ulinganishi, unaotumika kusisitiza sifa fulani alizo nazo mtu au kitu kinachoelezwa. Unaposoma au unaposikia tahsibiha unapiga taswira ya ‘shimo la panya’ (kwa mfano), nah ii inakusaidia kujua jambo fulani kuhusu tundu la pua. Katika kuchambua tashibiha hii zaidi, unajiuliza: ‘tundu la panya li vipi? Ni kubwa kabisa (kulinganisha na tundu la pua). Kuna giza ndani. Kumejaa viota vilivyokaa ovyoovyo na ni kuchafu. Hapo tutaweza kuona waziwazi zaidi mshairi anavyofikiri kuhusu pua ya mtu aliyelengwa.

Tashibiha ni ulinganishi wa wazi. Kwa maneno mengine, mwandishi au msemaji yuko wazi kuhusu ukweli kwamba huu ni ulinganishi. Baadhi ya maneno yanayoashiria tashibiha ni ‘kama’, mathalani: ‘Tundu la pua yako ni kama shimo la panya’ au ‘ Katika shimo la chini kwa chini, kulikuwa ni kweusi kama usiku’.

Kama mshairi angeandika ‘Tundu la pua yako ni shimo la panya’, hii ingekuwa na athari inayofanana nayo, lakini ulinganishi wa namna hii unaitwa sitiari. Hapa ulinganishi ni wa mdokezo. Hatuambiwi kuwa ulinganishi unafanyika. Tundu la pua linaelezwa kama kwamba ni tundu la panya.

Chanzo cha awali: Machin, N. African Poetry for Schools: Book 1

Nyenzo-rejea 2: Mfano wa somo