Nyenzo-rejea 2: Mfano wa somo

Taarifa ya usuli / maarifa ya somo kwa mwalimu

Mwalimu (M) anawafundisha wanafunzi (W) wa darasa la 7 Kiingereza (somo la kusoma) (Mwanafunzi = Mw)

M:     Ninalotaka kufanya sasa ni kwamba nitasoma kwanza, na nitawaomba mnifuate. Sawa?

W:    Ndiyo.

M:     Hapo zamani za kale, Mfalme wa Misri alitaka kufahamu jinsi watu wake walivyoishi. Misri iko wapi?

Mw:  Kaskazini mwa Afrika.

M:        Mnakubali? Mnakubali?

W:Ndiyo (Kwa pamoja).

M:     Sawa. Usiku mmoja alivaa kama mtu fukara na kuenda jijini. Jiji ni nini?

Mw: Mji…

M:     Aliwasikiliza watu wake wakilalamika. Watu wake walikuwa wakilalamika. Unapolalamika … ni kwamba huwa hujaridhika na hali ilivyo…

Mw:  Kutoridhika…

M:     Ndiyo, kutoridhika…niendelee na hadithi?

W:Ndiyo.

M:     Basi watu walisema kuwa walikuwa masikini na chakula kilikuwa ghali…Walilalamika…Hakuna aliyecheka katika jiji hili. Hakuna aliyeimba nyimbo, na hakuna aliyekuwa na furaha. Kila mtu alikuwa na huzuni… Mfalme alipokuwa akirejea kwenye ikulu yake… Ikulu ni nini?

Mw:       Ikulu ni mahali anapokaa mfalme.

M:     Vyema. Hadithi inaendelea…

Alipita karibu na kijiduka. Akasikia mtu akiimba. Ndani ya kijiduka. Aliingia ndani. Kijana mwanamme alikuwa amekaa sakafuni, akishona viatu, huku akiimba.

Mshona-viatu alipoona kwamba kuna mgeni, alisimama na kumsalimu. Kisha akampa mfalme mkate na maji. Alimpa nini?

W:    Mkate na maji.

M:     Je, mshona-viatu alifahamu kuwa huyu alikuwa mfalme? Kwa hakika, hakufahamu. Kwa nini hakufahamu?

Mw: Alivaa kama mtu fukara.

M:     Turudi kwenye hadithi. Hebu fikiria picha ya Madiba akiwa amevaa nguo kuukuu.…Unapata picha ya jambo ninalozungumzia?

W:    Ndiyo.

M:     Je, utamfahamu Madiba akitokea mlangoni hapo?

W:        La.

M:     La, hakuna anayeweza kumjua?

Mwalimu aliendelea kusoma hadithi na wanafunzi, akiwauliza maswali kuhusu hadithi hiyo. Maswali mengi yalikuwa yanafanana na hayo ya juu. Wanafunzi waliyajibu kwa ufupi, kwa Kiingereza. Kisha somo liliendelea kama lilivyoelezwa katika Uchunguzi-kifani 2.

Imetoholewa kutoka: Umthamo 3, Mradi wa Elimu-Masafa wa Chuo Kikuu cha Fort Hare

Nyenzo-rejea ya 1: Shairi

Nyenzo-rejea 3: Usalama