Nyenzo-rejea 3: Usalama

Nyenzo za mwalimu kwa ajili ya kupanga na kutumia na wanafunzi

Kaka yangu

Kaka yangu ni Ipyana Mwakipesile. Ana umri wa miaka 18, na ni kama baba kwangu. Baba yangu alikufa zamani sana. Ana nafasi muhimu sana katika maish ayetu, ingawa bado ni kijana anayesoma kidato cha tano Shule ya Sekondari Azania. Ni muwajibikaji. Anatutunza. Anapika chakula na kusafisha nyumba. Anamlea mtoto mchanga kwa sababu mama yetu aliaga dunia miezi michache iliyopita. Kila adhuhuri hufunga lango la ua ili tuwe salama ndani. Anatusaidia kwa kila njia. Hatujihisi kuwa mama yetu pia hayupo nasi. Kaka yetu hutupatia upendo ambao tulizoea kuupata kutoka kwa wazazi wetu. Kila Jumamosi, anaoka keki, anafanya manunuzi kama mama alivyokuwa akifanya. Kaka yangu ni kama baba kwetu. Tunamwamini, tunampenda.

Baba yangu

Baba yangu alizaliwa na kukulia Mbeya; baadaye akahamia Dar. Alisomea Shule ya Sekondari ya Minaki; mama yake alikufa baada yamiaka miwili. Baba yake alimwacha na wadogo zake wawili wa kike. Aliishi na babu na bibi, kisha akaishi na shangazi yake, kabla kuhamishiwa kwenye kituo cha watoto yatima.

Wakati akiwa katika kituo cha watoto yatima, alikabiliwa na shida nyingi na alijifunza mengi. Alipambana na watu wajeuri na mara nyingi ilimpasa kuwalinda dada zake. Ingawa alionekana kuwa na muda mgumu, alithamini yote aliyopata kituoni. Jambo gumu kuliko yote lilikuwa kutokuwa na familia yake.

Kutokana na malezi katika kituo cha mayatima, alijifunza kujikimu.

Akiwa ngazi ya juu ya Shule ya Sekondari, alifanywa kuwa kiranja mkuu. Alikuwa maarufu pia, na alishiriki katika shughuli mbalimbali za kitamaduni na riadha pia.

Alipomaliza shule, alijiunga na jeshi la kujenga taifa, na kuona sehemu nyingi za Tanzania. Mara nyingi husimulia hadithi na matukio aliyoshiriki wakati akiwa jeshini. Tajiriba zake katika kituo cha mayatima zilimsaidia kuyamudu maisha ya jeshini, na alikuwa kwenye kundi la viongozi, na akawa mkufunzi. Baba yangu daima amekuwa na marafiki wema na maalumu, na daima amekuwa katika nafasi fulani ya uongozi. Baada ya kumaliza mafunzo na huduma ya kijeshi, alikwenda kuchukua mafunzo ya ualimu.

Akiwa chuoni, alikutana na msichana ambaye baadaye alikuwa mtu muhimu sana katika maisha yake. Baada ya kumaliza masomo, alimposa. Uhusiano huu haukuendelea. Ni wakati huu ambapo mama alikuja kufanya kazi shule moja na baba. Walishikana urafiki na baadaye akamwoa.

Mwaka 1990 nilizaliwa, na tangu hapo nimekuwa karibu naye sana.

Baba yangu amekuwa na nafasi muhimu katika maisha yangu, na ninataka siku moja kurithisha tuzo aliyonipa. Amekuwa mwalimu wangu, kocha wangu wa michezo ya riadha, mshauri wangu, na juu ya yote, rafiki yangu wa karibu.

Imetoholewa kutoka ‘Children First’ Nov/Dec 2004/ Vol 8 No 58, ukurasa wa 5, 6, na 7

Nyenzo-rejea 2: Mfano wa somo

Nyenzo-rejea 4: Kauli za Dira na Malengo - mifano