Nyenzo-rejea ya 1: Namba mraba
Nyenzo ya Mwalimu kwa ajili ya kupanga/kurekebisha na kutumia na wanafunzi
Kwanza chora umbo mraba ubaoni na kuandika sm 2 katika pande zake na ligawanye katika miraba ya sm 1 kama inavyooneshwa.
Mwamuzi/jaji wa kwanza ahesabu mraba wa sm 1 na kuandika hii namba.
Mwandishi wa kwanza achore umbo mraba la sm 3 na pia aligawe katika maumbo mraba ya sm1 na rekoda ahesabu na kurekodi maumbo mraba hayo madogo.
Shughuli hii inaendelea kwa umbo mraba la sm 4, sm 5 na sm 6.
Mifano
Hapa kuna namba-mraba:
Waambie wanafunzi wawili wawili wachore namba mraba nyinginezo hadi mia moja. Wanafunzi hao wawili wawili hupeana zamu za kuchora na kuhesabu/kurekodi namba hizo.
Somo la 3