Somo la 2

Utakapolifahamu darasa lako itakusidia kuongea nao kuhusu sifa zao binafsi, vitu wanavyoweza kufanya, wanavyovipenda na wasivyovipenda pamoja na mazuri na mapungufu waliyonayo. Njia nzuri ya kufupisha haya majadiliano waambie wanafunzi wachore kwa uangalifu picha zao wenyewe na kuzionyesha kwa rangi moja sifa zao za pekee. Wanaweza kutumia rangi nyingine kuorodhesha na kurekodi sifa zingine walizo nazo.

Sasa watakuwa tayari kufanya kitu kimoja watakapo fikiria juu ya vitu vyenye tofauti za kawaida (aina za maada) wanazozijua kutoka katika mazingira yao. Katika Shughuli 2 chunguza njia moja ya kufanya hili, kwa kutumia picha 

Uchunguzi kifani 2, mwalimu anatambulishe wazo la tabia na hali tatu za maada (yabisi, kimiminika na gesi) kwa kuanzia na tabia moja-mgandamizo . Je hii ni tofauti na jinsi ulivyozoea kuanza mada? Je ni mada zipi zingine unazoweza kuchunguza kwa kutumia mkabala huu?

Uchunguzi kifani ya 2: Kulinganisha mgandamizo

Neema anashughulika na wanafunzi wa darasa la nne na alipanga kuwasilisha kwao wazo la hali tatu za mabadiliko ya maada yabisi, kimiminika na gesi. Lakini hakutaka kuwaambia

Kwa uangalifu aliandaa somo kwa kuzunguka wazo la mgandamizo. Aliwaonyesha sponji Aliwaonyesha sponji ndogo, tufe la pamba, kipande laini cha nguo cha mraba (kama kitambaa cha njano cha kufutia vumbi), maji na kipande cha ubao mgumu kila kimoja kwa wakati wake. Neema alionyesha namna ya kukamua, kulazimisha au kuvibonyeza chini katikati ya nafasi iliyobonyea ya ngumi iliyokunjwa. vitu vyote isipokuwa maji na kipande cha mbao. Hawezi kubadili kiurahisi ukubwa au umbo la mbao na ingawa anaweza kubadili umbo la maji, hawezi kubadili ukubwa wake.

Alifuatilia hili na somo ambalo alitumia sindano kuonyesha mgandamizo katika vimiminika kwa kulinganisha na yabisi (mchanga) na hewa (angalia Nyenzo rejea 2: Andalio la somo )

Shughuli ya 2: Kutumia ishara kuvitambua na kuviainisha vitu

Kufanya hili Shughuli kwa darasa zima, unatakiwa kutafuta bango utakaloweka chumbani kuonyesha msambao wa vitu tofauti (kwa mfano duka, kliniki au jiko).

Kwa kazi za kundi utahitaji picha kubwa kwa kila kundi- tumia picha tofauti kwa kila kundi (angalia picha katika magazeti na katalogi.) Matumizi ya picha mbalimabli yanampa mwanafunzi sababu ya kweli ya kutoa ripoti kwa sababu kila kundi lina habari/taarifa tofauti za kuchangia.

Wewe na wanafunzi wako chagua picha tatu zinazofaa kutumika katika somo hili. utahitaji ishara kuwakilisha yabisi (pengine picha ya tofali au mche mraba wa kahawia au nyeusi), kimiminika (yaweza kuwa tone la bluu) na gesi (yaweza kuwa wingu la matone ya kiwiti au risasi ).

Wanafunzi wachore hizi sanamu katika kipande cha mabaki ya kadi au kama inawezekana wakate maumbo na kuyapaka rangi kisha watumie sanamu ndogo ya ukanda unaonata kuweka alama ya yabisi, kimiminika, na gesi .

Hamasisha majadiliano na majibu toka katika kila kundi. Je wametambuaje kimiminika? Wametambuaje gesi? Angalia Nyenzo rejea 3: Mfano wa kazi za wanafunzi .