Somo la 3

Hapa, tunategemea kazi mbili za mwanzo kwa kushughulikia njia ambazo maada inaweza kubadilishwa:

mabadiliko rejevu- yanajulikana kama mabadiliko ya kimaumbile mabaadiliko ya yasiyobadilika (mabadiliko ambayo siyo rahisi kuyageuza) –

yanaitwa mabadiliko ya kikemikali.

Nta inayeyushwa na moto kisha inagandishwa tena hili ni badiliko la kimaumbile/kiumbo. Sukari iliyoyeyushwa inaweza kurudishwa tena ikiwa kimiminka kitageuka kuwa mvuke, pia hii ni badiliko la kiumbo. ( Nyenzo rejea 4: kupotea kwa barafu kidonge cha barafu inathibitisha wazo moja kwa darasa kuhusu badiliko la kiumbo) lakini siyo rahisi kioo kuweza kurudishwa kuwa mchanga hivyo hili ni badiliko la kikemikali

Uchunguzi kifani 3 unaonesha kuwa wanafunzi wanaweza kupata vipingamizi katika kufikiri kuhusu mabadiliko ya kikemikali. kupitia maonyesho ya mwongozo ( angalia Nyenzo rejea muhimu: kutumia maelezo na maonesho kusaidia kujifunza iwapo chuma na chuma cha pua kilichopata kutu( mabadiliko ya kikemikali) metali ikipoteza umbo lake na urefu. Katika Shughuli muhimu umetumia mashindano kuwafanya wanafunzi wako wafikirie kuhusu ni jinsi gani wanaweza kupunguza mwendo wa mabadiliko haya ya kikemikali

Uchunguzi kifani ya 3: Kuonesha mabadiliko yasiyo ya kiumbo

Yusufu ni mwalimu asiye na sifa anayejitolea katika shule ya kijiji chake. Anaamini kuwa kujifunza ni muungano wa vichekesho na kwa dhati. Ilipofikia wakati wa kuangalia mabadiliko yasiyo ya kiumbo aliandaa kazi kadhaa

Kwanza, alionyesha kilichotokea wakati kipande cha mkate mwishoni mwa waya kiliposukumwa kwenye kizibo cha mkono kinachomwa kwenye kipande cha mkaa kilichoungua kwenye moto uliotanda. Aliwaambia wanafunzi wake wachunguze kwa makini. Hatimaye mkate ulikauka kiasi cha kushika moto na kuungua na moto unaowaka. Kisha aliuliza: ni kipindi gani uliacha kuwa mkate? Unafikiri ni nini kimetokea? Ni kitu yabisi gani tutabaki nacho endapo tutayasaga mabaki hayo hadi yageuke kuwa unga? Baadhi ya wanafunzi walishasikia kuhusu kaboni na walielezea kuwa hiki ndicho kilichobakia. Aliungunza kipande cha ubao na kuwaonyesha pia kuwa iliyobaki ni kaboni pia. Alisikiliza kwa makini majibu yao na kuhamasisha maswali yaliyojikita katika uchunguzi wao. Kwa njia hii anaweza kupima kujifunza na kufikiri kwao.

Baadaye, aliwaonyesha dhahiri mabadiliko ya kikemikali. Alichanganya unga wa asidi ya tatari na unga wenye sodiamu bikaboneti na kuonyesha kuwa hakuna mabadiliko yaliyotokea. Lakini, kisha aliongeza maji na kuwaambia wachunguze. Hii ilizua maswali mengi. Kwa nini sauti ya mapovu na kuwa na mapovu. kuna nini kwenye mapovu? Ni gesi gani inayotolewa? Je kitu kimebadilika? Ikiwa tungeyeyusha maji tungepata nini? Aliongelea jinsi gani kitu kipya kimetengenezwa. Kwa maelezo zaidi angalia Nyenzo rejea 5: Molekyuli na Atomu .

Mwalimu Yusuph alimaliza somo kwa kuwaagiza wanafunzi wake kila mmoja atafute mifano mitatu ya badiliko la kikemikali kwa ajili ya somo la kesho. Alifurahia mifano waliyotoa –baadhi ya wanafunzi walileta vitu na kuonyesha jinsi gani vimebadilika.

Shughuli muhimu: Kupunguza mwendo kasi wa mabadiliko ya kikemikali

Waonyeshe darasa baadhi ya metali ambazo zimepata kutu. Waaulize ni wapi zimeonekana kuwa na kutu? Nini kinafanya chuma au chuma cha pua kupata kutu? Hili ni aina gani la badiliko? Kisha waambie changamoto yao ni kuchunguza jinsi ya kufanya chuma kisipate kutu.

Wagawe wanafunzi wako katika makundi. Wape kila kundi msumari wa chuma (au vipande vingine vidogo vidogo vya msumari) na uwaambie kusafisha misumari kwa msasa

Kisha waulize ni jinsi gani wataikinga misumari isipate kutu. Wanatakiwa kupanga uchunguzi wao; nini watafanya, vifaa watakavyo hitaji na kufanya ubashiri wao. Wanafikiri ni kwa nini wamepewa misumari miwili?

Siku inayofuata, waambie wanafunzi wapange vifaa vyao. Utatakiwakuwapangia muda wa kufanya uchunguzi wao kwa majuma/wiki chache zinazofuata. Baada ya majuma/wiki chache, waambie kila kundi kutoa taarifa za uchunguzi wao. Je njia zao zilifanikiwa? Ni wapi lazima njia hizo zitumike?

Nyenzo ya 1: Kutengeneza kitabu cha zigizaga