Nyenzo-rejea 3: ‘Ni nini kinachonyanyua ndege?’ Zoezi la vitendo la kufanya na wanafunzi wako.

Nyenzo ya Mwalimu kwa kupanga au kubadili nyenzo ili zitumike na wanafunzi.

Walimu wa Shule ya Sekondari ya Tambaza walimpa Mwalimu Paulina notisi zilizorudufiwa kutoka semina ya shule za msingi ambayo walihudhuria.

Maelezo haya yameandikwa hapo chini kwa ajili yako. Paulina na wanafunzi wake waliyafanyia kazi maelezo hayo; walivutiwa na kuendelea kuuliza maswali zaidi.

Moja kati ya maswali ambayo wanafunzi waliyauliza ni ni nini kinachotunza kitu kizito kama ndege kwenye hewa? Hili hakika ni swali zuri. Walimu wao walielezea kwamba kuna vitu mbalimbali vinavyoweza kuelezea kwa vitendo jinsi gani ndege inavyonyanyuliwa juu. Lakini inahitaji maelezo yanayotolewa kwa uangalifu zaidi.

Njia moja ya kupata fikra za wanafunzi ni kulinganisha mipasuko wa mipira kwa vifaa viwili. Unahitaji bomba la plastiki na bomba la chooni na puto vilivyotumika. Puliza puto kuelekea juu. Waulize wanafunzi nini kitakuwa kifaa bora cha kupulizia puto? Halafu waache wajaribu.

Sasa hiki ni kitu cha kufikiria kwa sababu matokeo yake hayatabiriki. Nini kinatokea kwenye bomba linaloshikiria mpira chini kwa nguvu?

Inaweza kuwa ni hewa tu. Mwalimu mwingine alitupa kazi nyingine ya vitendo kujaribu. Weka daraja la karatasi kwa kukunja sehemu mbili. Tumia jani kupitisha hewa chini ya daraja.

Ni nini unacho kibashiri kwamba kinaweza kutokea? Kinatokeaje? Kwa nini daraja linaporomoka ndani na siyo nje? La tatu jaribu kukunja karatasi ya A4 kutoka katikati, na baadaye gundisha kidogo pembeni mwishoni mwa karatasi kutengeneza bawa la ndege. Puliza kidogo kutokea pembeni na angalia nini kitatokea. Kifani/model ya karatasi litainuka.

Dondoo

Fikiria kundi la watu wanaotembea kando ya barabara. Wanasikia kitu cha hatari pembeni mwao na wanaanza kukimbia. Je nini kitatokea kwenye mpangilio wa watu?

Ndiyo wanafanya kusambaa kadri mwendo kasi wao unavyoongezeka

Jaribu kitu hicho hicho kwa mkono uliojaa marumaru. Kwanza zizungushe kwenye sura iliyonyooka na huwa zinatabia ya kuungana pamoja. Kisha zizungushe kwa kasi kubwa zaidi na zitasambaa.

Wakati hewa inalazimishwa kuzunguka haraka juu kwenye sura iliyopinda au kupitia nafasi nyembamba, chembe chembe zinasambaa nje. Hii ina maana kwamba kuna shinikizo dogo. Hivyo unaweza msukumo wenye nguvu au kuinyanyua kutoka kwenye hewa kwenda upande mwingine.

Ni muhimu kuchunguza na kulinganisha vitu hewani vinapoanguka toka angani. Kwanza tulijaribu riadha ya makaratasi. Tulilinganisha karatasi mbili zinazofanana, tulizilebo A na B, zikianguka angani. Kwa nini karatasi iliyokunywa huanguka haraka? Kwa kutafuta maneno rasmi ya kuelezea uchunguzi huu katika kitu bapa, tuliweza kuona jinsi uwepo wa lugha nyingi ni mzuri.

Karatasi A (bapa) Huelea

Hutikisika

Huzamia

Huyumba, kama unyoya Karatasi ya B (imekunjwa) Huanguka

Hunyooka 

Haraka

Huanguka, kama jiwe

Chanzo: Programu ya Sayansi ya Shule ya Msingi Daraja 4 Ripoti ya Warsha ya Hewa

Nyenzo-rejea ya 2: Utafiti wa Hewa

Nyenzo-rejea 4: Mashindano ya Karatasi