Nyenzo-rejea ya 2: Mazao ya mafuta machafu
Nyenzo ya Mwalimu kwa kupanga au kubadili nyenzo ili zitumike na wanafunzi.
Mchoro huu unaonyesha usafishaji wa mafuta.
Chanzo asili cha mchoro: Oxford Science Programme Book1, published by Oxford University Press, p. 92 (1990))
Matumizi ya mafuta machafu | |
Sehemu ya mafuta machafu | Mazao toka katika sehemu hii ya mafuta machafu (wakati mwingine baada ya kusafishwa) |
Gesi (G) | Mafuta ya gesi, kama gesi ya kala, kutengeneza kemikali nyingine |
Petroli (P) | Mafuta ya magari, madawa ya wadudu, madawa, maplastiki, mbolea za viwandani, nakishi, viyeyushi, kutengeneza kemikali zingine |
Mafuta ya taa (K) | Mafuta ya taa, mafuta ya ndege, spiriti nyeupe |
Dizeli (D) | Mafuta ya malori na mabasi, mafuta ya kuongeza joto |
Mafuta mazito (HO) | Mafuta ya kulainishia mitambo na grisi, nta, nakishi, kutengeneza kemikali zingine waxes, polishes, making other chemicals |
Mabaki (R) | Lami za barabarani, viziba maji, vifaa vya mapaa, mafuta ya mitambo |
Mawazo ya kufundishia
Mawazo ya kufundishia yaweza kuwa kuweka mabango ya mazao na mazao ya pembeni ya mafuta ghafi katika magazeti na matangazo ya majarida (unaweza onyesha mazao au majina ya kibiashara na nembo). Njia mbadala ni, unaweza kuzionyesha bidhaa katika makopo matupu. Mazao ya kuzingatia ni mafuta ya taa, dizeli, petroli, mishumaa, vesilini, mafuta ya kulainisha mitambo, lami, na maplastiki.
Mafuta na gesi katika nchi ya Tanzania
Tanzania imejaliwa kuwa na vyanzo tele vya nishati ikiwa ni pamoja na nishati ya kibaiolojia, gesi asilia, nishati ya maji, makaa ya mawe, nishati ya miamba, nishati ya jua, na nishati ya nafuta na vyote vikiwa bado havijaendelezwa. Nishati ya kuni inachukua asilimia 92 ya vyanzo vyote vya nishati, na asilimia 2 ni nguvu ya maji na asilimia 7 inatokana na mazao ya pembeni ya mafuta.
Katika shughuli kuu za sekta ya madini (yaani uchimbaji wa madini), utafutaji na utengenezaje wa mafuta na gesi pia unatiwa moyo. Maeneo makubwa ya mafuta yamepatikana katika upwa wa bahari huko Songo Songo na Rasi ya Mnazi na maeneo haya yapo katika hatua ya kuyaendeleza.
Sekita ya kaboni ya kihadrijia inaratibiwa na Wizara ya Nishati na Madini, ikiratibiwa shughuli zake kuu na Sheria ya Uchunguzi wa Mafuta ya mwaka 1980 na ikiratibiwa shughuli zake ndogondogo na Sheria ya Uvutiaji Uwekezaji ya mwaka 1990.
Akiba ya mafuta katika Tanzania, kwa njia ya kiseismiki au data zinginezo, inaonyesha kuwa kuna mafuta ya kaboni mengi sana katika vyanzo vya mafuta na katika sekita ya viwanda. Lakini, ni mitambo 20 tu na visima nane tu vimechimbwa katika eneo la kilomita mraba 222,000, kwa hiyo basi Tanzania inawekwa katika kundi la nchi zilizoendelezwa kidogo
Kwa sasa akiba ya gesi asilia inakadiliwa kuwa futi za mraba trilioni 2. Serikali inashughulikia kwa ukaribu na Benki ya Dunia kuendeleza mradi wa gesi wa Songo Songo huko kusini mwa ukanda wa bahari wa Tanzania na katika rasi ya Mnazi, ili kuweza kuweka chanzo mbadala dhidi
matumizi makubwa ya kuagiza mafuta toka nje. Mradi wa kugeuza gesi kuwa umeme wa Songo Songo utakuwa na soko la viwanda na watumiaji
17 wa gesi asilia katika eneo la Dar es Salaam.
Makampuni yanayochunguza kuwepo kwa akiba ya mafuta Tanzania ni: Kampuni ya Nishati ya PanOcean, Aminex plc na EnerGulf.
Chanzo: Taarifa za Afrika kutoka Mbendi , Website
Nyenzo-rejea ya 1: Rasilimali zinazorejelezwa na zisizorejelezwa