1. Kutambua Leba ya Kawaida

Kipindi cha 1 cha somo Kutambua Leba ya Kawaida

Utangulizi

Kwa kawaida, mhudumu mmoja wa afya ndiye anayefuatilia mwanamke mjamzito na mtoto wake tangu kuzuru kliniki ya wajawajazito hadi baada ya kuzaa. Jambo hili huitwa ufuatilizi wa huduma. Ulisoma moduli kuhusu huduma ya Kabla ya Kuzaa. Sasa utajifunza kuhusu Utunzaji wa Leba na Kuzaa. Leba nijina linalopewa mabadiliko ya kianatomi na kifisiolojia katika mkondo wa uzazi wa mwanamke. Mabadiliko haya hufanyika ili kutayarisha fetasi na plasenta kwa utaratibu wa kuzaa. Mara nyingi, leba hutokea wakati mtoto ameumbika kikamilifu, kufikia hatima ya wakati anaofaa kukaa mwilini mwa mama, yaani kati ya wiki 37-40 za ujauzito. Leba huashiria mwisho wa kipindi cha mtoto kukaa uterasini na mwanzo wa maisha nje ya mwili wa mama.

Kipindi hiki cha kwanza cha somo kinatanguliza moduli ya Utunzaji wa Leba na Kuzaa. Lengo kuu ni kukusadia kubainisha kati ya leba halisi na ile bandia. Utajifunza kutambua dalili za awamu nne za leba. Utajifunza kuhusu leba na utaratibu wa kuzaa ili uweze kufanya uamuzi sahihi na uwe na ujasiri unapozalisha. Pia utajifunza namna ya kumtayarisha mwanamke mjamzito kutambua mabadiliko mwilini mwake yanayoashiria kuwa leba iko karibu kuanza. Utajifunza jinsi ya kumwelimisha juu ya kutambua mwanzo wa leba halisi ili aweze kutafuta msaada wako kwa wakati unaofaa.

Matokeo ya Somo la Kipindi cha 1