11. Kuvuja Damu baada ya Kuzaa

Kipindi cha 11 Kuvuja Damu baada ya Kuzaa

Utangulizi

Takriban wanawake 127,000 kote duniani hufa kila mwaka kutokana na kuvuja damu baada ya leba na kuzaa. Hali hii hujulikana kama kuvuja damu baada ya kuzaa. Hali hii ni kisababishi kikuu cha vifo vya kina mama vinavyohusiana na kuzaa, nayo husababisha robo ya vifo vyote vya kina mama vinavyohusiana na kuzaa. Kila mwaka, visa milioni 14 vya kuvuja damu hutokea wakati wa ujauzito na kuzaa. Hali hii hutokea mara nyingi kwa sababu uterasi haikujikaza vyema baada ya plasenta kutoka. Katika Kipindi cha 6, ulijifunza kuhusu jinsi ya kudhibiti awamu ya tatu ya leba. Awamu ya tatu ya leba huanza kwa kuzaliwa kwa mtoto na kukamilisha kutoa kwa plasenta na membreni za fetasi.

Katika kipindi hiki, utajifunza kuhusu kuvuja damu baada ya kuzaa na jinsi ya kuidhibiti hali hii. Kuvuja damu baada ya kuzaa ni hali hatari zaidi inayohitaji matibabu ya dharura. Hatua zako za haraka zinaweza kuokoa maisha ya watu wengi. Usisahau kuwa kuvuja damu baada ya kuzaa (kuvuja damu kupita kiasi kabla ya leba kuanza) kunaweza kuhatarisha maisha ya mama na mtoto. Ulijifunza kuhusu kuvuja damu nyakati za mwanzo na za mwisho wa ujauzito katika Kipindi cha 20 na 21 cha Moduli ya Utunzaji wa Wakati wa Ujazito.

  • Je, unaweza kukumbuka vipengele viwili ambavyo mara nyingi husababisha kuvuja damu katika kipindi cha mwisho wa ujauzito?

  • Vipengele viwili ambavyo mara nyingi husababisha kuvuja damu katika kipindi cha mwisho wa ujauzito ni privia ya plasenta na kutengeka kwa plasenta. Privia ya plasenta hutokea wakati plasenta imekaribia seviksi au kuifunika. Plasenta hujitenga seviksi inapoanza kupanuka wakati leba inapoanza. Kutengeka kwa plasenta hutokea plasenta inapokuwa katika pahali pake pa kawaida katika thuluthi mbili za juu ya uterasi, lakini imetengeka kabla ya mtoto kuzaliwa.

    Mwisho wa jibu

Malengo ya Somo la Kipindi cha 11