3. Kumtunza Mama aliye katika Leba

Kipindi cha 3 Kumtunza Mama aliye katika Leba

Utangulizi

Katika kipindi kilichopita cha Moduli hii, ulijifunza kuhusu ufasili, ishara na dalili, na awamu za leba ya kawaida. Leba na kuzaliwa kwa mtoto ni tukio la kipekee katika maisha ya familia yoyote na pia huwa na umuhimu wa namna ya kipekee kwa mama binafsi. Kushirikiana na mwanamke mjamzito na umahiri wako katika kudhibiti utaratibu wa kuzaliwa huchangia kuwepo kwa hali ya kuridhisha pamoja na uaminifu wakati wa leba na kuzalisha. Hisia hizi huchangia katika matokeo bora. Ni lazima uwe msikivu unapomtunza mwanamke aliye katika leba. Ni lazima uelewe mahitaji yake na jinsi mama yule anavyofahamu leba.

Katika kipindi hiki utajifunza jinsi ya kumfadhili mwanamke katika kipindi chote cha kuzaa. Pia utapewa utangulizi wa kanuni za kimsingi za ufuatilizi wa mama na fetasi wakati wa leba. Utajifunza pia kuhusu kiwango cha usafi kinachohitajika ili kuzuia maambukizi na pia kuhusu vifaa unavyopaswa kutayarisha ili kuzalishia nyumbani au katika kituo cha afya.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 3