5. Kutekeleza Uzalishaji wa Kawaida

Kipindi cha 5 Tekeleza Uzalishaji wa Kawaida

Utangulizi

Katika masomo ya vikao vya awali, ulijifunza ufafanuzi, dalili na hatua za leba. Ulijifunza jinsi ya kutumia patografu. Aidha ulijifunza jinsi ya kumtunza mjamzito aliye katika leba. Katika Kipindi hiki, utajifunza jinsi ya kumsaidia mjamzito aliye katika hatua ya pili ya leba ya kawaida na jinsi ya kumtoa mtoto. Katika hatua ya pili ya leba, mama humsukuma mtoto chini kutoka kwenye uterasi kuelekea kwa uke na mtoto huzaliwa. Hatua ya pili huanza wakati seviksi ipanukapo kabisa. Hatua hii ya pili hukamilika mtoto azaliwapo.

Mjamzito haonyeshi hisia kwa muda mrefu katika hatua ya kwanza ya leba. Katika hatua ya pili, hali hiyo hubadilishwa na nguvu kali za mwili zitumikazo kwa muda mfupi. Mjamzito na msaidizi wake wawe na ushupavu, uvumulivu na matumaini kutoka kwa mkunga. Lazima utoe huduma bora na uwe na uhusiano nzuri na mama.

Malengo ya Somo la Kipindi cha 5